Sunday, January 31, 2010

Misri Yaibanjua Ghana na Kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika


Timu ya taifa ya Misri imefanikiwa kulitwaa kombe la mataifa ya Afrika kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kuwabanjua vijana wa Ghana kwa bao 1-0 katika mechi ya fainali jijini Luanda, Angola.
Ghana imeshindwa kwa mara nyingine kumaliza kiu ya miaka 28 ya kombe la mataifa ya Afrika baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 toka kwa mabingwa watetezi Misri.

Alikuwa ni mchezaji wa akiba wa Misri Mohamed Gedo aliyeingia uwanjani dakika ya 70 na kufanikiwa kulifumania lango la Ghana kwenye dakika ya 85.

Gedo aliachia shuti ndani ya 18 lililojaa nyavuni na kuifanya Misri iweke historia ya kulitwaa kombe la Mataifa ya Afrika kwa mara ya saba.

Misri pia imeweka rekodi ya kulitwaa kombe hilo mara tatu mfululizo. Hakuna timu nyingine iliyowahi kufanya hivyo.

Wawakilishi wa Afrika kwenye kombe la dunia nchini Afrika Kusini, Ghana waliitawala mechi ya leo lakini washambuliaji wake walishindwa kuzifumania nyavu za Misri.

Ikiingiza uwanjani wachezaji wanne wa timu ya taifa ya vijana ya Ghana ya chini ya miaka 20 ambayo ilitwaa kombe la dunia mwaka jana, Ghana ilifanikiwa kuliandama lango la Misri kwenye kipindi cha kwanza lakini viungo wake walishindwa kuwachezesha vizuri washambuliaji wake.

Asamoah Gyan, mshambuliaji wa Ghana aliyeipatia Ghana magoli ya ushindi katika mechi dhidi ya Angola na Nigeria alikaribia kuifumania nyavu ya Misri kwenye dakika ya 52 lakini shuti lake lilipanguliwa na golikipa wa Misri, El Hadary.

Hatimaye Gebo ambaye amekuwa mfungaji bora wa mashindano haya kwa kufunga magoli matano, aliwasononesha Ghana kwenye dakika ya 85 kwa kuachia shuti lililojaa kwenye nyavu za kushoto za kipa wa Ghana, Richard Kingson.

Katika mechi ya kutafuta mshindi wa tatu iliyochezwa kabla ya mechi ya fainali, Nigeria ilifanikiwa kuwalaza Algeria 1-0 na kunyakua ushindi wa tatu.


source nifahamishe

Manchester Yaizamisha Arsenal 3-1


nchester United imetamba kwenye uwanja wa Emirates jijini London na kuwabugiza wenyeji Arsenal magoli 3-1.Manchester United imepunguza pengo la pointi kati yake na vinara wa ligi ya Uingereza, Chelsea kwa kuibanjua Arsenal magoli 3-1 kwenye uwanja wake wa Emirates.

Winga wa Manchester United toka Ureno, NANI ndiye aliyekuwa mwiba mkali kwa mabeki wa Arsenal katika mechi ya leo.

Katika dakika ya 35, Nani baada ya kuwaramba chenga wachezaji watatu wa Arsenal alimimina majaro kati lakini kipa wa Arsenal, Manuel Almunia, aliusindika mpira huo kwenye nyavu zake katika harakati za kuuokoa.

Dakika nne baadae Nani tena alimpa pasi nzuri sana Wayne Rooney ambaye hakufanya ajizi kuiandikia Manchester goli la pili ambalo lilikuwa ni goli lake la 100 katika ligi ya Uingereza.

Mkorea Park Ji-Sung alipigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Arsenal kwenye dakika ya 52 baada ya kuambaa na mpira karibia nusu ya uwanja na kuachia shuti lililojaa kwenye ubavu wa kulia wa nyavu za Arsenal.

Wakati washabiki wa Arsenal wakianza kutoka uwanjani dakika 15 kabla ya mechi kuisha, Thomas Vermaelen aliipatia Arsenal goli la kufutia machozi kwenye dakika ya 80.

Akiongea baada ya kichapo hicho, kocha wa Arsenal, Arsene Wenger aliwataka wachezaji wake kukusanya nguvu zao tena na kulipa kisasi kwa kuilaza Chelsea watakapokutana siku ya jumapili.


source nifahamishe

Friday, January 29, 2010

Reds reject new Babel bid


The Blues have been tracking the Reds winger since the opening of the January transfer window but saw a reported £9 million bid rebuffed by the Merseyside giants at the start of the month.

Liverpool chief Rafael Benitez claimed Babel still had an integral to play at Anfield, but the 23-year-old has made just one substitute appearance since City's offer.

Babel, who announced his displeasure at being left out of a recent Liverpool squad on Twitter before apologising personally to Benitez, was originally not keen on a move to St Andrews.

But the player's agent has since revealed the Dutch international had a change of heart, with the World Cup on the horizon, but it appears Alex McLeish's latest bid to lure the former Ajax star to the West Midlands has been shunned.

Blues could still bring Aruna Dindane to the Second City, however, despite reports that the deal has fallen through.

Dindane was in Birmingham on Friday after the Blues agreed a £4 million deal for the Ivory Coast marksman but the move was believed to have broken down due to the player's demands.

But skysports.com understands a deal for the Lens striker - on loan at Portsmouth - is not completely dead in the water and talks are still ongoing.

City also remain confident on signing Roman Pavlyuchenko despite seeing a substantial offer turned down by Tottenham on Friday

The Russian striker appears to be McLeish's number one target before Monday's deadline

source skysport

Chama cha riadha Zanzibar chataka kuandaa riadha taifa

CHAMA cha Riadha Zanzibar (ZAAA) kimeomba kuandaa mashindano ya Taifa ya mchezo huo kwa mwaka huu yanayotarajia kufanyika mwezi Mei.

Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania, RT, Suleimani Nyambui alisema tayari wamepokea mwaliko kutoka ZAAA kuhusiana na maombi hayo.

Alisema maombi ya ZAAA yatajadiliwa katika kikao cha Kamati ya Ufundi ya RT kabla ya kutolewa uamuzi.

"ZAAA wametuletea barua hapa kuomba kuandaa mashindano ya Taifa bila shaka wameshawishika kufanya hivyo baada ya kuufanyia ukarabati Uwanja wa Amani hususani ile sehemu ya kukimbilia pamoja na ile saa ya kurekodi muda wa kukimbia," alisema Nyambui.

Mara ya mwisho Zanzibar iliandaa mashindano ya riadha ya Taifa mwaka 1971.


source mwananchi

Kenya, Tanzania kuandaa fainali za Afrika 2014

SHIRIKISHO la Soka Kenya, KFF limeomba Shirikisho la Soka Afrika uenyeji wa Fainali za Afrika 2016 na kuiteua Tanzania na Uganda kuunganisha nguvu kuandaa kwa pamoja.

Taarifa ya KFF ambayo Mwananchi imeipata, ilisema kuwa kwa muda mrefu shirikisho hilo limepeleka maombi CAF kutaka uenyeji huo huku likijinadi kujitosheleza kwa miundombinu.

"Baada ya mkutano wetu kwa pamoja, Job Omino (mwenyekiti wa taifa), Sam Obingo (katibu) na James Tirop kwa mara ya kwanza tuliomba haya kwa Fainali za 1996. Hata hivyo, Afrika Kusini ndiyo ilikuwa mwenyeji.

Hata hivyo, serikali kupitia kwa Waziri wa Michezo, James Njiru alipinga hatua hiyo ya KFF lakini baada ya ujio wa wawakilishi kutoka shirikisho la soka Afrika CAF na kuishauri Serikali umuhimu wa kuandaa michuano hiyo wengi walikubaliana na kauli hiyo ingawa wengine walipinga lakini shirikisho hilo likasimama na kutetea nafasi hiyo.

KFF haikukata tamaa na ilibidi kuwasilisha michoro ya viwanja ikiwemo wa Mombasa, Moi Kasarani na City na CAF iliridhishwa na hatua hiyo na kuitaka Kenya kuendelea kujipanga.

Baadaye CAF ilimtuma mjumbe wake, Farah Addo kwenda kikagua viwanja pamoja na kuwa na mazungumza na Waziri wa sasa wa Michezo, Maalim Mohamed na katika mazungumzo yao, walizungumzia jinsi gani wanaweza kuufanyia ukarabati Uwanja wa Mombasa ambao nao ungeweza kutumika kwa fainali hizo.

Sasa, pamoja na kwamba Afrika Kusini inataka kuwa mwenyeji wa Fainali za 2016, lakini tangu kuingia kwa Job Omono katika Chama cha FORDKENYA mpango wake ni kuunganisha kupitia soka ambao morari ya soka imepotea.

"Tunataka kuandaa Fainali za 2016 na endapo inashindikana, mpango wetu ni kuandaa kwa pamoja na Tanzania, Uganda na Zanzibar," ilisema taarifa ya KFF.

CAF wasiwe na wasiwasi na Kenya kama tukishinda,

lazima Bunge liidhinishe fedha ili vijengwe viwanja vitatu vya kisasa na pia lazima itolewe barua ya idhini ya Rais kuruhusu fainali hizo bila kujali yeyote atakayeshinda urais katika uchaguzi wa 2012.

Hata Kenya ikikosa kama Kenya lazima ujumbe wa Afrika Mashariki kupitia Rais wa TFF na CECAFA, Leodegar Tenga lazima kuipenyeza na kuipigia debe hoja ya Afrika Mashariki kuwa mwenyeji wa Fainali za 2016.

CAF inaweza kuangalia wazo la kuandaa kwa pamoja nchi za Afrika Mashariki kwa kuwa kila nchi tajwa kuna viwanja vya kisasa katika miji ya Nairobi, Dar es Salaam na Kampala. Zanzibar inaweza kutumika pia.

Timu 16 zitagawanywa katika mataifa manne ya Afrika Mashariki na mechi tisa zitachezwa kila nchi hatua ya makundi, pamoja na mechi za robo fainali zitachezwa katika miji ya Nairobi, Kampala, Dar es Salaam na Zanzibar.

Mechi za mshindi wa tatu, nusu fainali na fainali zitafanyika katika nchi ambazo waandaaji watakubaliana kati ya Nairobi, Dar es Salaam na Kampala.

Mawasiliano ni mazuri Afrika Mashariki, viwanja bora vinavyohitaji ukarabati mdogo, vivutio vya utalii, hoteli za kisasa, mashabiki wanaweza kusafiri kwa barabara kwenda kwenye mechi bila vikwazo.

Wakati huo huo, CAF imesema kuwa mechi za ufunguzi kwa Fainali za Afrika 2012 zitakazoandaliwa kwa pamoja kati ya Gabon na Guinea ya Ikweta itachezwa Guinea ya Ikweta wakati fainali itachezwa Gabon.

source nifahamishe

Ghana hiyoo fainali, Yaichapa NIgeria 1-0


GHANA 'Black Stars' imeingia fainali ya Fainali za Afrika baada ya miaka 28 baada ya Asamoah Gyan kupachika bao pekee la kichwa lililoizamisha Nigeria.

Gyanalifunga bao hilo katika dakika ya 21 na kuipeleka fainali Black Stars ikiwa ni mara ya kwanza tangu 1992.

Timu hiyo yenye tiketi ya Kombe la Dunia itakuwa ikisubiri Algeria au Misri zilizokuwa zikicheza jana usiku kwenye mji wa Benguela.

Hadi tunakwenda mitamboni mpambano huo ulikuwa unaendelea.

Nigeria sasa inasubiri mwenzake atakayeshindwa katika mchezo huo ambao watakutana kesho kutafuta mshindi wa tatu na nne. Fainali itachezwa hapa keshokutwa.

Katika mchezo Obinna Nwaneri alifanya kazi ya ziada kuzuia mpira wa dhabu wa Asamoah Gyan uliotoka na kuwa iliyozaa bao.

Kona hiyo ilipigwa na Kwadwo Asamoah na kumkuta ndugu yake, Asamoah Gyan aliyejitwika kichwa kuandika bao hilo pekee la Black Stars.

Bao hilo liliwapa nguvu Waghana na kuendelea kulishambulia kwa nguvu lango la wapinzani wao wakiongozwa na Gyan na Opoku Agyemang.

Hata hivyo, Danny Shittu na Elderson Echiejile walifanya kazi ya kumzuia.

Katika dakika ya 25, Gyan alikosa bao la wazi akiwa na kipa wa Nigeria, Vincent Enyeama ambaye alimuwahi kabla ya kuupiga mpira huo.

Kipindi cha pili, Nigeria ilianza kwa kufanya mashambulizi ya mfululizo, katika dakika za 75, 76 na 77.

Washambuliaji wa timu hiyo, Yakubu Aiyegbeni aliyeingia kuchukua nafasi ya Peter Odemwingie na Obafemi Martins walikuwa mwiba, lakini mashambulizi yao yaliishia kwenye ukuta wa Ghana.

Kuona hali inazidi kuwa nzito, ilimtoa Yusuf Ayila na nafasi yake kuchukuliwa na Obinna Nsofor wakati Ghana ilimtoa, Hans Sarpei aliyeumia na nafasi yake kujazwa na Rahim Ayew.

Wakati huo huo, mbali na kufungwa, wachezaji wa Nigeria wamepatiwa bonasi zao zilizotokana na harambee ya Rais wa nchi hiyo, PTF.

Habari zilizopatikana jana zilisema kuwa Shirikisho la Soka (NFF) liliwalipa asilimia 50 wachezaji hao wakati kamati ya hamasa ya Rais iliwapa asilimia nyingine 50.

Kabla ya kucheza nusu fainali, kila mchezaji wa Nigeria alikuwa na dola30,000 kwa kuingia robo fainali na dola 12,500 kwa kuichapa Zambia 5-4.

Kabla ya PTF kuwapa fedha hizo, maofisa wa NFF waliwaambia wachezaji kutuliza akili zao na kuhakikisha wanafika mbali katika fainali hizo kabla ya kupigwa bao 1-0 na Ghana.

Kocha wa Ghana, Milovan Rajevac alisema kuwa vijana wake wameonyesha kiwango cha hali ya juu hapa Angola.

Alisema kuwa kila mechi wamekuwa wakiimarika na kinachoangaliwa kwa sasa ni kutwaa ubingwa wa Afrika

"Nilichukua wachezaji wanane wa U-20 waliotwaa Kombe la Dunia na wameonyesha kweli wanaweza," Rajevac alisema.

source mwananchi

Nahodha wa Uingereza Ajivinjari na Mpenzi wa Mchezaji Mwenzake


Nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza na timu ya Chelsea ya jijini London, John Terry ambaye ana mke na watoto wawili alijivinjari na mpenzi wa mchezaji mwenzake wa Chelsea na alipogundua siri imefichuka alikimbilia mahakamani kuchukua kibali cha kuwazuia waandishi wa habari kufichua siri hiyo.
John Terry nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza na timu ya Chelsea, mume na baba wa watoto wawili, aliisaliti ndoa yake na kutembea na mpenzi wa mchezaji mwenzake Wayne Bridge aliyekuwa akiichezea Chelsea kabla ya kuhamia Manchester City.

John Terry aliposhtukia waandishi wa habari wamelinyaka soo hilo, alikimbilia mahakamani kuchukua kibali cha kuwazuia waandishi wa habari kuandika habari hiyo kwenye magazeti.

Kibali hicho kilitolewa kwa muda lakini leo pingamizi la mahakama liliondolewa na hivyo magazeti kuwa huru kumuandika John Terry alivyoisaliti ndoa yake na kumla uroda mpenzi wa rafiki yake.

Taarifa zinasema kwamba Terry alianza kujivinjari na mpenzi wa Wayne Bridge mrembo wa Ufaransa, Vanessa Perroncel, baada ya Wayne Bridge kuhama Chelsea na kuhamia Manchester City mwezi januari mwaka jana.

Vannessa ambaye ni mama wa mtoto mmoja wa kiume wa Wayne Bridge mwenye umri wa miaka mitatu, alibakia jijini London wakati Wayne Bridge alihamia mjini Manchester.

Wayne Bridge na Vannesa waliachana mwezi uliopita.

Hili ni skendo la pili kumkumba John Terry, mwaka 2003 alitiwa mbaroni kwa kupigana kwenye ukumbi wa starehe lakini baadae aliachiwa huru.

Wazazi wake nao ni maarufu magazetini kwa maskendo yaliyozua maswali mengi na kumtia aibu milionea John Terry.

Wakati mama yake alikamatwa akiiba nguo kwenye supermarket, baba yake alinaswa akiuza madawa ya kulevya.


source nifahamishe

Thursday, January 21, 2010

Tevez slams 'idiot' Neville


Manchester City striker Carlos Tevez has branded Gary Neville an 'idiot' and admits his goal celebration in the Carling Cup was directed at his former team-mate.

The Argentina international scored twice against Manchester United in a fiery semi-final first leg at Eastlands on Tuesday, putting City in the driving seat going into next week's game at Old Trafford as they claimed a 2-1 win.

Tevez netted City's equaliser from the penalty spot three minutes before half-time, and he ran to the touchline to exchange gestures with United fans' favourite Neville during his celebration.

Tevez made a gesture for Neville to keep his mouth shut before cupping his hands behind his ears, in response to comments from Neville that he was not worth the money City spent on him, and the defender then hit back with a rude gesture.

The 25-year-old, who moved from United to City for £25.5million last summer, admits he had to contain himself in his celebration, but revealed he was directing his actions towards Neville.

"In all the press here, Gary Neville came out and stood by (Sir Alex) Ferguson's comments, saying that I wasn't worth 25million," he told Argentinean radio.

"I thought he was in the wrong because we were team-mates and I never disrespected him, I always respected him.

"I feel he was a boot-licker when he stood by Ferguson's comments that I wasn't worth that money.

"From a former team-mate it hurts, from a coach it doesn't surprise me.

"I would never do that gesture towards the fans, I would never show a lack of respect towards people. It was directed at Gary Neville.

"Just as I was running off to celebrate the penalty I had scored, I came across Gary and I said to myself, 'shut your trap, keep quiet'.
Overboard

"I didn't go overboard in my celebration and it was directed at Gary, not at Ferguson and not at the fans. I didn't even look at Ferguson.

"You have to do your talking on the pitch. I know that Ferguson loves me, that's why he always talks about me."

The former Boca Juniors, Corinthians and West Ham striker admits he was upset when he first heard of Neville's newspaper comments.

"I was the first to sit down to have lunch in the team hotel and all the papers were laid out," he added.

"I looked at them as, although I couldn't read them, there were (photos) of Gary Neville and they were talking about me.

"Then I asked my team-mates what it said.

"I thought to myself, 'what's this idiot talking about me for when I never said anything about him, when there was never any (problems) with us?'

"It was a lack of respect for a (former) team-mate, aside from the fact that we had won a lot of things together.

"Thank God I had the chance to get revenge with City, although there is still the second leg to come."

source skysports