Wednesday, March 31, 2010

Arsenal Chupu Chupu Kuzamishwa na Barcelona


Arsenal imenusurika chupu chupu kupokea kichapo toka kwa Barcelona na kuzalimisha sare ya bao 2-2 kwenye uwanja wake wa Emirates. Katika mechi nyingine ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya, Inter Barcelona ikitandaza soka ambalo liliwafanya wenyeji Arsenal waonekane kama wageni kwenye uwanja wao wa Emirates, ilishindwa kuyalinda magoli yake mawili na kukubali kutoka sare ya bao 2-2 na vijana wa Arsene Wenger.

Hata hivyo Barcelona bado inapewa nafasi kubwa ya kusonga mbele katika mechi ya marudiano jumanne ijayo kutokana na faida ya magoli mawili ya ugenini na kuumia kwa wachezaji watatu tegemezi wa Arsenal, Cesc Fabregas, William Gallas na Andrey Arshavin.

Barcelona ilianza kwa kasi kubwa sana mechi hiyo na kuifanya Arsenal itumie muda mwingi ndani ya nusu ya uwanja wake kulilinda lango lake.

Kipa wa Arsenal, Manuel Almunia alikuwa mkombozi wa Arsenal kwenye kipindi cha kwanza kutokana na jinsi alivyookoa mashambulizi makali ya Barcelona.

Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa sare ya bila kufungana.

Kipindi cha pili kilianza kwa Zlatan Ibrahimovic kuiandikia Barcelona goli la kwanza sekunde chache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili. Ibrahimovic aliongeza goli la pili kwenye dakika ya 59.

Kuingia kwa Theo Walcott kwenye dakika 65 ya kuliongeza kasi ya mashambulizi ya Arsenal na alikuwa ni Walcott aliyeipatia Arsenal goli la kwanza dakika 69.

Kwenye dakika ya 85, nahodha wa Barcelona, Puyol alimkwatua Fabregas ndani ya 18 na kupelekea penalti ambayo iliwekwa kimiani na Fabregas mwenyewe kabla hajatoka nje ya uwanja akichechemea.

Arsenal sasa italazimika kuifunga Barcelona au kutoka sare ya mabao zaidi ya mawili ili kuweza kusonga mbele.

Katika mechi nyingine ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya, Inter Milan iliibanjua CSKA Moscow 1-0 kwenye uwanja wa San Siro.
iliifunga CSKA Moscow 1-0.

source nifahamishe

Maradona Aharibiwa Sura Yake na Mbwa Wake


Diego Maradona aliwahishwa hospitali na kufanyiwa operesheni ya dharura kurekebisha sura yake baada ya kung'atwa vibaya na mbwa wake alipojaribu kumbusu.
Madaktari nchini Argentina walilazimika kumfanyia operesheni ya dharura gwiji wa soka duniani, Diego Maradona ambaye alijeruhiwa vibaya na mmoja wa mbwa wake.

Maradona alishonwa nyuzi 10 kwenye mdomo wake wa juu baada ya kung'atwa na mbwa wake mwenye sura ya kutisha anayeitwa Bela ambaye ni jamii ya mbwa wa kichina wanaoitwa Shar-Pei.

Inadaiwa kuwa Maradona alijaribu kumbusu ili kumliwaza mbwa wake huyo aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya tumbo ndipo mbwa huyo kwa hasira alipomshambulia mdomoni.

Maradona alipata majeraha makubwa kwenye mdomo wake wa juu na alikimbizwa hospitali huku akivuja damu nyingi.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari, Maradona atalazimika kupumzika kwa siku tatu baada ya kutumia masaa 15 hospitalini.

Maradona hakuzungumza na waandishi wa habari lakini Fernando Molina, mpenzi wa dada yake Maradona, Dalma, aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa Maradona anaendelea vizuri na amepumzika nyumbani kwake.

Maradona aliwahi kulazwa kwenye hospitali hiyo hiyo mwaka 2007 kutokana na maradhi aliyopata kutokana na unywaji pombe uliokithiri.

Maradona mwenye umri wa miaka 49 ndiye anayetarajiwa na Waargentina kuiongoza timu ya taifa ya Argentina kulinyakua kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Maradona alichaguliwa kuwa kocha wa Argentina mwaka 2008 baada ya kujiuzulu kwa kocha Alfio Basile.

Pamoja na Argentina kutoonyesha uwezo mkubwa katika mechi za hatua ya awali ya kufuzu fainali ya kombe hilo, hatimaye ilifanikiwa kupata tiketi ya kuja Afrika baadae mwaka huu.

Argentina ipo kundi moja na Nigeria pamoja Ugiriki na Korea Kusini.

source nifahamishe

Thursday, March 25, 2010

Messi Amuovateki Beckham Kwa Kuchukua Mshiko Mkubwa


David Beckham sio tena mcheza soka anayelipwa pesa nyingi kuliko wote kwani hivi sasa nyota wa Barcelona, Lionel Messi ndiye yupo kwenye chati anaingiza mshiko mkubwa zaidi kwa mwaka kuliko wachezaji wote duniani.
Lionel Messi nyota wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina ndiye mchezaji anayekamata mshiko mkubwa zaidi kwa mwaka kuliko wachezaji wote duniani.

Kwa mwaka, Messi anajiingizia kiasi paundi milioni 29.6 ambazo ni milioni 2.3 zaidi ya anazoingiza David Beckham.

Kwa mwaka Messi anapokea mshahara wa paundi milioni 9, analipwa bonasi ya paundi milioni 3.6 na anaingiza paundi milioni 17.1 kutokana na matangazo ya makamapuni mbali mbali kama vile adidas, Pepsi na Gillette.

Katika listi ya wachezaji 10 wanaojiingizia kipato kikubwa kwa mwaka, nyota wa Cameroon, Samuel Et'oo anashika nafasi ya 10 kwa kiasi chake cha paundi milioni 12.4.

Hata hivyo wachezaji wa soka bado hawajafanikiwa kuwaovateki kwa kipato wachezaji wa mpira wa kikapu na gofu.

Tiger Woods ndiye mwanamichezo anayeingiza mshiko mkubwa kuliko wanamichezo wote duniani, anayemfuatia ni mchezaji mwenzake wa gofu Phil Mickelson huku nyota wa mpira wa kikapu, LeBron James akishika nafasi ya tatu.

Orodha kamili ya wanasoka 10 wenye kipato kikubwa kwa mwaka ni kama ifuatavyo:
1. Lionel Messi (Barcelona) £29.6m

2. David Beckham (LA Galaxy) £27.3m

3. Cristiano Ronaldo (Real Madrid) £26.9m

4. Kaka (Real Madrid) £16.9m

5. Thierry Henry (Barcelona) £16.2m

6. Ronaldinho (AC Milan) £15.4m

7. Carlos Tevez (Manchester City) £13.8m

8. Zlatan Ibrahimovic (Barcelona) £13m

9. Frank Lampard (Chelsea) £12.7m

10. Samuel Eto’o (Inter Milan) £12.4m


source nifahamishe

Monday, March 22, 2010

Manchester United Yaikong'oli Liverpool 2-1


Manchester United imerudi tena kileleni mwa ligi ya Uingereza baada ya kufuta uteja wake kwa Liverpool kwa kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye uwanja wa Old Trafford jijini
VIDEO - Manchester United Yaikong'oli Liverpool 2-1


Wachezaji wa Manchester United wakipongezana Sunday, March 21, 2010 7:55 PM
Manchester United imerudi tena kileleni mwa ligi ya Uingereza baada ya kufuta uteja wake kwa Liverpool kwa kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye uwanja wa Old Trafford jijini Manchester. VIDEO za magoli yote katika mechi hii mwisho wa habari hii.
Matumaini ya Liverpool kutwaa nafasi ya nne katika msimamo wa ligi ya Uingereza ili kuweza kucheza kombe la mabingwa wa ulaya msimu ujao yamezidi kufifia baada ya kupoteza pointi zingine muhimu kwa Manchester United.

Liverpool iliingia uwanjani ikiwa na nia ya kuiharibia Manchester United kampeni yake ya kutwaa ubingwa wa Uingereza kwa mara 19 na hivyo kuivuka rekodi ya Liverpool ya mataji 18.

Iliwachukua dakika tano tu Liverpool kuweza kupata goli la kuongoza kupitia kwa Fernando Torres ambaye aliunganisha vyema krosi ya Dirk Kuyt na kumwacha kipa wa Manchester United, Edwin van der Sar aking'ang'aa macho.

Manchester United ilipewa penalti dakika tano baadae baada ya Javier Mascherano kumuangusha Antonio Valencia kwenye mstari wa 18. Wayne Rooney alipiga penalti hiyo ambayo iliokolewa na kipa wa Liverpool, Pepe Reina lakini mpira ulipomrudia tena Rooney hakufanya ajizi kuuzamisha nyavuni.

Jahazi la Liverpool lilizama kwenye dakika ya 15 ya kipindi cha pili wakati Park Ji-sung alipopiga mbizi na kuunganisha kwa kichwa krosi ya Gary Neville.

Goli hilo lilidumu hadi wakati refa wa mechi hiyo alipopuliza kipyenga cha kumaliza mpambano huo
source nifahamishe

Friday, March 19, 2010

Arsenal Kukumbana na Barcelona, Manchester na Bayern Munich


Heka heka za robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya zitaendelea tena wiki mbili zijazo kwa mabingwa watetezi Barcelona kupimana ubavu na Arsenal huku Manchester United ikitimua vumbi na Bayern Munich.
Ratiba ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya imetangazwa leo kwa timu ya Arsenal ya Uingereza kupangiwa mabingwa watetezi Barcelona ambao hivi sasa wanatisha kwa boli wanalolitandaza.

Manchester United itajaribu kukumbukia maajabu yake ya mwaka 1999 kwa kupimana ubavu na wababe wa bundesliga Bayern Munich.

Vijana wa Jose Mourinho, Inter Milan watatoana jasho na CSKA Moscow kuwania nafasi ya nusu fainali huku Lyon ya Ufaransa iliyoitupa nje ya mashindano Real Madrid, itakutana na ndugu zao Bordeaux.

Mechi za kwanza za robo fainali zitachezwa wiki mbili zijazo machi 30 na machi 31 huku mechi za marudiano zikipangwa kufanyika aprili 6 na 7.

Ratiba ya robo fainali inamfanya nyota wa Barcelona, Thierry Henry arudi uwanja wa Emirates kwa mara ya kwanza tangia alipouzwa kwa Barcelona mwaka 2007 kwa dau la paundi milioni 16.

Arsenal ambayo itacheza mechi ya kwanza nyumbani, itajaribu kulipa kisasi cha kichapo ilichopewa na Barcelona miaka minne iliyopita wakati ilipolazwa 2-1 na Barcelona kwenye mechi ya fainali wakati huo Thiery Henry akiichezea Arsenal.

Akizungumzia uwezo wa Barcelona kwa timu za Uingereza, Thiery Henry alisema kuwa Barcelona ipo kwenye chati ya juu sana hivi sasa na nyota wa Barcelona,Muargentina, Lionel Messi ndiye mtu atakayeharibu ndoto za timu za Uingereza kunyakua kombe la mabingwa wa ulaya.

source nifahamishe

Thursday, March 11, 2010

Didier Drogba ndio mwanasoka bora Afrika


Mchezaji matata wa Ivory Coast Didier Droga ameshinda tuzo la mwanasoka bora zaidi barani Afrika mwaka 2009.
Drogba alifunga mabao matano wakati Ivory Coast ilipofuzu kwa kombe la dunia na vile vile kuifungiaa klabu yake bao katika Mwenzake wa klabu hiyo Michael Essien na mchezaji wa Cameroon Samuel Eto'o waliteuliwa kuwania tuzo hiyo.

Drogba, aliyefikisha umri wa miaka 32, hapo jana, amewahi kushinda tuzo hiyo mwaka wa 2006.

Timu ya taifa ya Algeria ilitajwa kuwa timu bora zaidi mwaka huu katika sherehe iliyofanyika mjini Accra, Ghana. ya kombe la FA...


source gblp