Polisi wa nchini Austria wamemtia mbaroni mwanaume mmoja wa nchini humo ambaye alikuwa akifanya matukio ya uporaji pesa kwenye mabenki akiwa amevaa kinyago chenye sura ya rais wa Marekani, Barack Obama. | ||
| Taarifa ya polisi wa Vienna, Austria imesema kuwa mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 45 raia wa Ujerumani anatuhumiwa kupora pesa kwenye benki zipatazo 7 za nchini humo ambapo wakati wote alikuwa akivaa kinyago chenye sura ya Barack Obama. Polisi walisema kuwa tangu mwaka 2008, mwanaume huyo alifanya matukio 7 ya uporaji pesa kwenye mabenki na tukio lake la mwisho la uhalifu alilifanya mchana wa siku ya alhamisi katika kijiji cha Fornach. Msako wa polisi ulianza na alitiwa mbaroni muda mfupi baadae baada ya mbwa wa polisi kufanikiwa kukiona kinyago na silaha alizokuwa akizitumia jambazi huyo. Jambazi huyo alikiri kufanya matukio ya ujambazi na polisi walitangaza kuwa wana furaha wamemtia mbaroni jambazi waliyekuwa wakimtafuta kwa muda mrefu. | ||
source nifahamishe | ||
Sunday, April 3, 2011
Jambazi 'Obama' Atiwa Mbaroni
Thursday, June 10, 2010
Friday, June 4, 2010
Liverpool Yamtema Benitez

Baada ya Liverpool kuvurunda msimu uliopita na kumaliza ligi ikiwa imeshika nafasi ya saba, kocha wa Liverpool Rafa Benitez amepoteza kazi yake baada ya miaka sita ya kuiongoza Liverpool.
Rafa Benitez ametemwa na Liverpool baada ya miaka sita kufuatia kufanya vibaya kwa Liverpool katika msimu uliopita.
Liverpool ilimaliza ligi ikishika nafasi ya saba, ilitolewa mapema kwenye makombe ya Carling na kombe la FA, haikufika kokote kwenye kombe la mabingwa wa ulaya kabla ya kutolewa nusu fainali kwenye kombe la UEFA.
Liverpool imemlazimisha Benitez achukue mikoba yake kwa kukatisha mkataba wake na kumlipa fidia ambayo inakadiriwa kufikia paundi milioni sita.
Benitez mwenye umri wa miaka 50 alisema baada ya kujulishwa kuwa kibarua chake kimeota mbawa: "Nina huzuni sana kutangaza kuwa sitaendelea kuwa kocha wa Liverpool FC. Napenda kuwashukuru wafanyakazi wote na wachezaji kwa juhudi zao".
Mwenyekiti wa Liverpool, Martin Broughton aliongeza: "Rafa ataendelea kukumbukwa na Liverpool kwa kutuletea kombe la mabingwa wa ulaya katika fainali dhidi ya AC Milan mjini Istanbul".
Broughton aliongeza kuwa baada ya msimu ambao haukuwa na matokeo mazuri, Liverpool imeona ni bora ijijenge tena upya.
Mchakato wa kutafuta kocha mpya wa Liverpool umeanza.
source nifahamishe
Monday, May 31, 2010
Eto'o Atishia Kuitosa Cameroon Baada ya Kukosolewa na Roger Milla

Nyota wa timu ya taifa ya Cameroon, Samuel Eto'o ametishia kujitoa kwenye timu ya Cameroon itakayoshiriki kombe la dunia baada ya kukosolewa na mkongwe wa soka Afrika, Roger Milla.
Mshambuliaji wa Inter Milan Samuel Eto'o ametishia kususia kuichezea Cameroon baada ya kukosolewa na nyota wa Cameroon wa kombe la dunia la 1990, Roger Milla kuwa hajitumi anapoichezea timu ya taifa.
Akiongea hivi karibuni na vyombo vya habari, Roger Milla alimkosoa Eto'o akisema kuwa Eto'o hujituma zaidi anapoichezea yake ya Inter Milan kuliko anapoichezea timu yake ya taifa.
Akiongea na televisheni ya Canal Plus Sport ya Ufaransa, Eto'o alielezea kukasirishwa na maoni ya Roger Milla na kuongeza kuwa huenda akajitoa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon kitakachoshiriki fainali za kombe la dunia nchini Afrika Kusini.
"Kwani kombe la dunia ndio la muhimu sana kwangu?", alisema Eto'o.
"Bado nina siku chache za kufikiria nichukue uamuzi gani kwakuwa huwa sipendi mambo kama haya", aliongeza Eto'o.
"Roger Milla amefanya nini cha maana? amewahi kuchukua kombe la dunia? timu yake ya mwaka 1990 iliishia robo fainali", alisema Eto'o kwa hasira.
Hata hivyo pamoja na Eto'o kutishia kuitosa Cameroon, kocha wa Cameroon, Paul Le Guen alimtaja Eto'o kwenye kikosi chake cha wachezaji 23 kitakachoenda Afrika Kusini kwenye fainali za kombe la dunia.
Kikosi kamili cha Cameroon ni kama ifuatavyo:
Hamidou Souleymanou (Kayserispor), Carlos Kameni (Espanyol), Guy Roland Ndy Assembe (Valenciennes); Benoit Assou-Ekotto (Tottenham), Sebastien Bassong (Tottenham), Gaetan Bong (Valenciennes), Aurelien Chedjou (Lille), Geremi (Ankaragucu), Stephane Mbia (Marseille), Nicolas Nkoulou (Monaco), Rigobert Song (Trabzonspor); Eyong Enoh (Ajax), Jean II Makoun (Lyon), Georges Mandjeck (Kaiserslautern), Joel Matip (Schalke), , Landry Nguemo (Celtic), Alexandre Song (Arsenal); Vincent Aboubakar (Coton Sport), Eric Choupo-Moting (Nuremberg), Achille Emana (Betis), Samuel Eto'o (Inter Milan), Mohamadou Idrissou (Freiburg), Achille Webo (Mallorca).
source nifahamishe
Friday, May 28, 2010
Jose Mourinho Atua Real Madrid

Wababe wa Hispania Real Madrid, wamefanikiwa kumnyakua kocha wa mabingwa wa ulaya Inter Milan ya Italia, Jose Mourinho.
Baada ya kutwaa makombe matatu msimu huu, kocha wa Inter Milan, Jose Mourinho ameitosa timu hiyo na kuhamia kwa timu tajiri duniani ya Real Madrid ya Hispania.
Tovuti ya Real Madrid ilitoa taarifa leo kuwa makubaliano yamefikiwa kati ya Inter Milan na Real Madrid hivyo Mourinho ndiye atakayekuwa kocha mpya wa Real Madrid.
Awali kabla ya makubaliano hayo kufikiwa, Inter Milan iligoma kumuachia Mourinho ikitaka ilipwe fidia ya euro milioni 16 kwa Mourinho kukatisha mkataba wake ambao umebakiza miaka miwili.
Rais wa Real Madrid Florentino Perez alienda Milan kukutana na mwenyekiti wa Inter Milan Massimo Moratti ili kufikia muafaka juu ya suala hilo la Mourinho. hata hivyo maafikiano yaliyofikiwa na klabu hizo hayakuwekwa wazi.
Jose Mourinho atatambulishwa kwa wapenzi wa Real Madrid siku ya jumatatu saa saba mchana kwa saa za Tz kwenye uwanja wa Real Madrid wa Santiago Bernabeu.
source nifahamishe
Sunday, May 23, 2010
Inter Milan Ndio Mabingwa wa Ulaya, Yaibanjua Bayern 2-0

Kocha wa Inter Milan ya Italia Jose Mourinho akiingiza uwanjani kikosi ambacho hakikuwa na Muitaliano hata mmoja, amedhihirisha makali yake mbele ya bosi wake wa zamani kocha wa Bayern Munich, Louis van Gaal kwa kuigaragaza Bayern kwa mabao 2-0.
Internazionale Milano (Inter Milan) imekuwa mabingwa wapya wa ulaya baada ya kuwatungua Bayern Munich kwa magoli 2-0 katika mchezo wa fainali ya mabingwa wa ulaya iliyochezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu.
Inter Milan imechukua kombe leo ikiwa ni miaka 45 tangia ilipochukua mara ya mwisho kombe barani ulaya. Wakati huo kocha wake Jose Mourinho alikuwa na umri wa miaka miwili. Leo Mourinho akiwa na umri wa miaka 47 ameiwezesha Inter Milan kurudi katika anga la soka la ulaya na kuwa mabingwa wapya wa ulaya.
Ingawa Inter Milan ni timu ya Italia lakini kocha wa Inter Milan Jose Mourinho hakumuingiza mchezaji hata mmoja toka Italia katika kikosi chake cha kwanza. Muitaliano pekee aliyecheza mechi ya leo alikuwa ni Marco Materazzi ambaye aliingia uwanjani dakika mbili kabla ya mechi kuisha.
Bayern Munich ingawa ilitawala mechi yote na kumiliki mpira muda mrefu walishindwa kuivunja ngome ya Inter Milan ambayo ilicheza kwa kujilinda zaidi staili ambayo Mourinho hupenda kuitumia anapokuwa katika wakati mgumu.
Magoli mawili ya Muargentina Diego Milito katika dakika ya 35 na 70 yaliiwezesha Inter Milan kuwa mabingwa wapya wa ulaya kwa msimu wa mwaka 2009-2010.
Jose Mourinho ambaye kuna uwezekano mkubwa akaikimbia Inter Milan msimu ujao kwenda kuifundisha Real Madrid, amemaliza msimu huu kwa kuiwezesha Inter Milan kutwaa jumla ya makombe matatu.
source nifahamishe
Sunday, May 16, 2010
Chelsea Yaibanjua Portsmouth na Kutwaa Kombe la FA

Mabingwa wa ligi ya Uingereza, Chelsea wameongeza kombe jingine kwenye hazina yake mwaka huu baada ya kuwabanjua Portsmouth kwa goli 1-0 kwenye fainali ya kombe la FA.
Goli lililofungwa na nyota wa mchezo Didier Drogba kwa mkwaju wa adhabu ndogo, liliiwezesha Chelsea kutwaa makombe mawili katika msimu mmoja kwa mara ya kwanza katika historia yake.
Kocha wa Chelsea ambaye alianza kuifundisha Chelsea mwanzoni mwa msimu ulioisha amemaliza msimu wake wa kwanza Uingereza akiwa amejikusanyia makombe matatu, kombe la ngao, kombe la ligi ya Uingereza na kombe la FA.
Katika mechi ya leo, Chelsea haikupata ushindi kirahisi kwani Portsmouth mbali ya kushuka daraja ilitandaza soka safi na kumweka kipa wa Chelsea, Petr Cech kwenye heka heka mara kwa mara.
Cech aliwanyima Portsmouth goli ambalo lingebadilisha muelekeo wa mchezo kwenye dakika ya 56, alipoipangua penalti iliyopigwa na nyota wa Portsmouth, Kevin Prince Boateng.
Kipa wa Portsmouth, David James ndiye aliyekuwa kwenye patashika muda wote kutokana na mashambulizi makali ya Chelsea yaliyoongozwa na Drogba.
Katika kipindi cha kwanza pekee, Chelsea waliwakosakosa Portsmouth ambapo mara tano mpira uligonga mwamba na kugoma kuingia nyavuni.
Kombe la leo limekuwa kombe la nane la nahodha wa Chelsea, John Terry tangu alipoanza kuichezea timu hiyo.
source nifahamishe
Tuesday, May 11, 2010
Nigeria Yatangaza Kikosi cha Kombe la Dunia

Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles ametangaza kikosi cha wachezaji watakaoiwakilisha Nigeria kwenye kombe la dunia mwezi ujao nchini Afrika Kusini bila ya kumsahau mtu mzima Nwanko Kanu.
Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria Lars Lagerback ambaye alikabidhiwa mikoba ya ukocha wa Nigeria baada ya kocha Shaibu Amodu kuvurunda kwenye fainali za kombe la mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Angola, ametangaza kikosi cha awali cha wachezaji 30 ambacho baadae kitachujwa na kubaki na wachezaji 23 watakoiwakilisha Nigeria kwenye fainali za kombe la dunia zinazoanza mwezi ujao.
Katika kikosi hicho Lars amemuita nyota wa Portsmouth ya Uingereza iliyoshuka daraja, mkongwe Nwanko Kanu.
Magolikipa watatu kati ya wanne walioitwa na kocha wa Nigeria wanacheza soka nchini Israel.
Kikosi kamili cha Nigeria ni kama ifuatavyo:
Magolikipa: Vincent Enyeama (Hapoel Tel Aviv, Israel), Dele Aiyenugba (Bnei Yehuda, Israel), Austin Ejide (Hapoel Petah Tikva, Israel), Bassey Akpan (Bayelsa United, Nigeria)
Mabeki: Taye Taiwo (Marseille, France), Elderson Echiejile (Rennes, France), Chidi Odiah (CSKA Moscow, Russia), Onyekachi Apam (OG Nice, France), Joseph Yobo (Everton, England), Daniel Shittu (Bolton Wanderers, England), Ayodele Adeleye (Sparta Rotterdam, Netherlands), Rabiu Afolabi (SV Salzburg, Austria), Terna Suswan (Lobi Stars, Nigeria)
Viungo: Chinedu Ogbuke Obasi (TSG Hoffenheim, Germany), John Utaka (Portsmouth, England), Brown Ideye (FC Sochaux, France), Peter Utaka (Odense Boldklub, Denmark), Kalu Uche (Almeria, Spain), Dickson Etuhu (Fulham, England), John Mikel Obi (Chelsea, England), Sani Kaita (Alaniya, Russia), Haruna Lukman (AS Monaco, France), Yusuf Ayila (Dynamo Kiev, Ukraine), Osaze Odemwingie (Lokomotiv Moscow, Russia)
Washambuliaji: Yakubu Aiyegbeni (Everton, England), Victor Anichebe (Everton, England), Nwankwo Kanu (Portsmouth, England), Obafemi Martins (Wolfsburg, Germany), Ikechukwu Uche (Real Zaragoza, Spain), Victor Obinna Nsofor (Malaga, Spain)
source nifahamishe
Monday, May 10, 2010
Chelsea Ndio Mabingwa wa Uingereza

Wazee wa darajani Chelsea wamekatisha matumaini ya Manchester United kutwaa ubingwa wa Uingereza kwa mara ya nne mfululizo baada ya kuunyakua ubingwa wa Uingereza kwa kutoa kipigo cha nguvu kwa Wigan kwa kuiburuza magoli 8-0.
Magoli manane waliyobugizwa Wigan Athletic leo kwenye uwanja wa Stamford Bridge yameiwezesha timu ya Chelsea kutwaa tena kombe la ubingwa wa ligi ya Uingereza kwa mara ya nne katika historia ya timu hiyo.
Ushindi wa magoli 4-0 ilioupata Manchester United dhidi ya Stoke City haukuweza kuwasaidia kunyakua taji la ligi ya Uingereza kwa mara ya 19.
Magoli matatu ya Didier Drogba kwenye kipindi cha pili yalimwezesha kuwa mfungaji bora wa ligi ya Uingereza kwa msimu wa mwaka 2009/2010.
Magoli mengine ya Chelsea katika ushindi wa leo yalifungwa na Nicolas Anelka, Salomon Kalou, Ashley Cole na Frank Lampard.
Kocha wa Chelsea amekuwa miongoni mwa makocha wachache sana katika ligi ya Uingereza ambao walifanikiwa kutwaa ubingwa katika mwaka wao wa kwanza wa kuanza kazi.
Chelsea sasa ina mpango wa kuongeza kombe jingine kwenye hazina yake mwaka huu wakati itakapopimana ubavu na Portsmouth kwenye mechi ya fainali ya kombe la FA itakayochezwa jumamosi ijayo kwenye uwanja wa Wembley.
source nifahamishe
Messi Kuvunja rekodi Ya Dunia Usajili Msimu Ujao

Nyota wa Argentina na timu ya Barcelona ya Hispania, Lionel Messi anatabiriwa kuvunja rekodi ya dunia ya usajili msimu ujao kwa jinsi timu tajiri za barani ulaya zinavyojiandaa kutoa donge nene kwa Barcelona ili kuwashawishi wamuuze nyota wao huyo.
Vyanzo mbalimbali vya habari vimeanza kumtabiria nyota wa klabu ya Barcelona Lionel Messi kuvunja rekodi ya dunia ya usajili pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa katika msimu ujao.
Habari zinasema tayari klabu mbalimbali za ulaya zimeanza mikakati ya kuitafuta saini ya messi huku nyingine zikianza kupiga hodi Barca zikiishawiwishi klabu hiyo kumuachia messi kwa gharama kubwa.
Miongoni mwa klabu ambazo zimeonyesha nia ya kutaka kuvunja akaunti yao benki ni Real Madrid matajiri wa hispania ambapo tayari wameshatangaza dau la kitita cha paundi miloni 120 kumng’oa nyota huyo Barcelona na kumuingiza Santiago Bernabeu.
Madrid ambayo msimu uliopita ilivunja rekodi ya dunia katika usajili wa mchezaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo ikilipa paundi milioni 80 sasa imedhamiria kuvunja rekodi nyingine kwa mchezaji huyo wa kimataifa Lionel Messi.
Mpango halisi wa Madrid ni kumngo’oa Messi kwa mkataba wa paundi milioni 120 ambapo unaonekana kuanza kufanyiwa kazi na maafisa wa klabu hiyo.
Lakini mpango huo umekuwa ukichukuliwa kwa hisia tofauti na klabu hiyo ya Barcelona ambapo inasemekana bado uongozi unajadili kuchukua fedha na kuuvunja mwamba au kuacha fedha na kuboresha ngome yao katika msimu ujao.
source nifahamishe
Thursday, April 22, 2010
Inter Milan Yaipasua Kichwa Barcelona
Vijana wa Jose Mourinho, Inter Milan wamewashindilia mabao 3-1 mabingwa watetezi Barcelona katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la mabingwa ulaya iliyochezwa usiku huu.
Mabingwa watetezi Barcelona ya Hispania ambayo iliigaragaza timu ya Arsenal ya Uingereza kwa jumla ya mabao 6-3 na kuitupa nje ya mashindano ya mabingwa wa ulaya, imeshindwa kutamba nchini Italia na kukubali kipigo cha mabao 3-1.
Barcelona ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuliona lango la Inter Milan dakika 18 tu baada ya kipyenga cha kuanza kwa mechi mfungaji akiwa ni Pedro.
Goli hilo liliwafanya vijana wa Mourinho waje juu na kujipatia goli la kusawazisha kupitia kwa Wesley Sneijder kwenye dakika ya 29.
Hadi wakati kipyenga cha mapumziko kinapulizwa, Barcelona na Inter walikuwa sare ya mabao 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi zaidi na walikuwa ni Inter Milan waliofanikiwa kujipatia magoli mawili ya haraka haraka kupitia kwa Maicon and Diego Milito.
Macho yote leo yalikuwa kwa mchawi wa chenga mwenye umbile dogo, Lionel Messi ambaye alifunga magoli manne peke yake katika mechi ya robo fainali dhidi ya Arsenal.
Lakini mabeki wa Inter Milan walifanikiwa kumbana Messi asifanye makeke yake yaliyompatia jina duniani.
Jose Mourinho hivi sasa ana kazi ngumu zaidi ya kuhakikisha anaiongoza vyema Inter Milan kulinda ushindi wake kwenye mechi ya marudiano itakayofanyika wiki ijayo kwenye uwanja wa Nou Camp nchini Hispania
source nifahamishe
Mabingwa watetezi Barcelona ya Hispania ambayo iliigaragaza timu ya Arsenal ya Uingereza kwa jumla ya mabao 6-3 na kuitupa nje ya mashindano ya mabingwa wa ulaya, imeshindwa kutamba nchini Italia na kukubali kipigo cha mabao 3-1.
Barcelona ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuliona lango la Inter Milan dakika 18 tu baada ya kipyenga cha kuanza kwa mechi mfungaji akiwa ni Pedro.
Goli hilo liliwafanya vijana wa Mourinho waje juu na kujipatia goli la kusawazisha kupitia kwa Wesley Sneijder kwenye dakika ya 29.
Hadi wakati kipyenga cha mapumziko kinapulizwa, Barcelona na Inter walikuwa sare ya mabao 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi zaidi na walikuwa ni Inter Milan waliofanikiwa kujipatia magoli mawili ya haraka haraka kupitia kwa Maicon and Diego Milito.
Macho yote leo yalikuwa kwa mchawi wa chenga mwenye umbile dogo, Lionel Messi ambaye alifunga magoli manne peke yake katika mechi ya robo fainali dhidi ya Arsenal.
Lakini mabeki wa Inter Milan walifanikiwa kumbana Messi asifanye makeke yake yaliyompatia jina duniani.
Jose Mourinho hivi sasa ana kazi ngumu zaidi ya kuhakikisha anaiongoza vyema Inter Milan kulinda ushindi wake kwenye mechi ya marudiano itakayofanyika wiki ijayo kwenye uwanja wa Nou Camp nchini Hispania
source nifahamishe
Monday, April 19, 2010
Skendo la Ngono Laikumba Timu ya Taifa ya Ufaransa

Skendo kubwa la ngono limeikumba timu ya taifa ya soka ya Ufaransa ambapo baadhi ya nyota wa timu hiyo ya taifa wanadaiwa kufanya mapenzi na machangudoa wenye umri mdogo.
Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya soka ya Ufaransa wamehusishwa kwenye skendo la kufanya mapenzi na makahaba wenye umri chini ya miaka 18.
Mchezaji nyota wa Ufaransa, Franck Riberry na Sidney Govou ni wachezaji wawili waliotajwa ambao tayari wameishahojiwa na polisi kuhusiana na skendo hilo.
Riberry anayeichezea Bayern Munich ya Ujerumani ana mke lakini naye amenaswa katika skendo hilo akidaiwa kufanya mapenzi na msichana kahaba mwenye umri chini ya miaka 18.
Taarifa zilisema kuwa wachezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa "Les Bleus" walikuwa wakienda sana kwenye klabu moja ya starehe ya jijini Paris ambapo walikuwa wakiandaliwa makahaba wenye umri chini ya miaka 18. Mmoja wa makahaba hao inadaiwa alikuwa na umri wa miaka 14.
Wachezaji wengine nyota wa Ufaransa nao wamehusishwa na skendo hilo lakini majina yao yamewekwa kapuni.
Mmoja wa wachezaji hao alikiri kufanya mapenzi na msichana mwenye umri mdogo lakini alijitetea kuwa wakati huo alikuwa akiamini kuwa mwanamke aliyeletewa ni mtu mzima.
Kuwadi "Pimp" anayedaiwa kuwaandalia wachezaji machangudoa hao ametiwa mbaroni na baadhi ya wasichana hao wanaendelea kuhojiwa na polisi.
Skendo hilo limekuja ikiwa ni miezi miwili tu kabla ya Ufaransa kuja barani Afrika kwaajili ya fainali za kombe la dunia.
source nifahamishe
Sunday, April 18, 2010
Tottenham Yaharibu Sherehe za Chelsea
Tottenham Hostspur ya jijini London imevuruga mahesabu ya wazee wa darajani Chelsea kutwaa ubingwa wa ligi ya Uingereza kwa kuizamisha kwa mabao 2-1 huku Manchester United ikiwazamisha watani wake wa jadi Manchester City kwa bao 1-0.
Vinara wa ligi ya Uingereza Chelsea leo wamepigwa mwereka na Tottenham Hotspur na kuzamishwa mabao 2-1 na hivyo kuyafanya matumaini ya Chelsea kutwaa ubingwa wa Uingereza mapema kuyeyuka.
Kabla ya mechi Chelsea ilikuwa ikiongoza ligi ya Uingereza kwa tofautiya pointi nne na Manchester United lakini kipigo cha Chelsea na kushinda kwa Manchester United dhidi ya watani wao wa jadi Manchester City kumelifanya pengo la pointi kati ya Chelsea na Manchester United kupungua hadi pointi moja.
Chelsea imebakiza mechi tatu dhidi ya Stoke City, Liverpool na Wigan na italazimika kushinda mechi zote ili kujihakikishia ubingwa.
Kwa upande wake, Manchester United imebakiza mechi tatu dhidi ya Tottenham, Sunderland na Stoke City.
source nifahamishe
Vinara wa ligi ya Uingereza Chelsea leo wamepigwa mwereka na Tottenham Hotspur na kuzamishwa mabao 2-1 na hivyo kuyafanya matumaini ya Chelsea kutwaa ubingwa wa Uingereza mapema kuyeyuka.
Kabla ya mechi Chelsea ilikuwa ikiongoza ligi ya Uingereza kwa tofautiya pointi nne na Manchester United lakini kipigo cha Chelsea na kushinda kwa Manchester United dhidi ya watani wao wa jadi Manchester City kumelifanya pengo la pointi kati ya Chelsea na Manchester United kupungua hadi pointi moja.
Chelsea imebakiza mechi tatu dhidi ya Stoke City, Liverpool na Wigan na italazimika kushinda mechi zote ili kujihakikishia ubingwa.
Kwa upande wake, Manchester United imebakiza mechi tatu dhidi ya Tottenham, Sunderland na Stoke City.
source nifahamishe
Wednesday, March 31, 2010
Arsenal Chupu Chupu Kuzamishwa na Barcelona

Arsenal imenusurika chupu chupu kupokea kichapo toka kwa Barcelona na kuzalimisha sare ya bao 2-2 kwenye uwanja wake wa Emirates. Katika mechi nyingine ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya, Inter Barcelona ikitandaza soka ambalo liliwafanya wenyeji Arsenal waonekane kama wageni kwenye uwanja wao wa Emirates, ilishindwa kuyalinda magoli yake mawili na kukubali kutoka sare ya bao 2-2 na vijana wa Arsene Wenger.
Hata hivyo Barcelona bado inapewa nafasi kubwa ya kusonga mbele katika mechi ya marudiano jumanne ijayo kutokana na faida ya magoli mawili ya ugenini na kuumia kwa wachezaji watatu tegemezi wa Arsenal, Cesc Fabregas, William Gallas na Andrey Arshavin.
Barcelona ilianza kwa kasi kubwa sana mechi hiyo na kuifanya Arsenal itumie muda mwingi ndani ya nusu ya uwanja wake kulilinda lango lake.
Kipa wa Arsenal, Manuel Almunia alikuwa mkombozi wa Arsenal kwenye kipindi cha kwanza kutokana na jinsi alivyookoa mashambulizi makali ya Barcelona.
Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa sare ya bila kufungana.
Kipindi cha pili kilianza kwa Zlatan Ibrahimovic kuiandikia Barcelona goli la kwanza sekunde chache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili. Ibrahimovic aliongeza goli la pili kwenye dakika ya 59.
Kuingia kwa Theo Walcott kwenye dakika 65 ya kuliongeza kasi ya mashambulizi ya Arsenal na alikuwa ni Walcott aliyeipatia Arsenal goli la kwanza dakika 69.
Kwenye dakika ya 85, nahodha wa Barcelona, Puyol alimkwatua Fabregas ndani ya 18 na kupelekea penalti ambayo iliwekwa kimiani na Fabregas mwenyewe kabla hajatoka nje ya uwanja akichechemea.
Arsenal sasa italazimika kuifunga Barcelona au kutoka sare ya mabao zaidi ya mawili ili kuweza kusonga mbele.
Katika mechi nyingine ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya, Inter Milan iliibanjua CSKA Moscow 1-0 kwenye uwanja wa San Siro.
iliifunga CSKA Moscow 1-0.
source nifahamishe
Maradona Aharibiwa Sura Yake na Mbwa Wake

Diego Maradona aliwahishwa hospitali na kufanyiwa operesheni ya dharura kurekebisha sura yake baada ya kung'atwa vibaya na mbwa wake alipojaribu kumbusu.
Madaktari nchini Argentina walilazimika kumfanyia operesheni ya dharura gwiji wa soka duniani, Diego Maradona ambaye alijeruhiwa vibaya na mmoja wa mbwa wake.
Maradona alishonwa nyuzi 10 kwenye mdomo wake wa juu baada ya kung'atwa na mbwa wake mwenye sura ya kutisha anayeitwa Bela ambaye ni jamii ya mbwa wa kichina wanaoitwa Shar-Pei.
Inadaiwa kuwa Maradona alijaribu kumbusu ili kumliwaza mbwa wake huyo aliyekuwa akisumbuliwa na maumivu ya tumbo ndipo mbwa huyo kwa hasira alipomshambulia mdomoni.
Maradona alipata majeraha makubwa kwenye mdomo wake wa juu na alikimbizwa hospitali huku akivuja damu nyingi.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari, Maradona atalazimika kupumzika kwa siku tatu baada ya kutumia masaa 15 hospitalini.
Maradona hakuzungumza na waandishi wa habari lakini Fernando Molina, mpenzi wa dada yake Maradona, Dalma, aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa Maradona anaendelea vizuri na amepumzika nyumbani kwake.
Maradona aliwahi kulazwa kwenye hospitali hiyo hiyo mwaka 2007 kutokana na maradhi aliyopata kutokana na unywaji pombe uliokithiri.
Maradona mwenye umri wa miaka 49 ndiye anayetarajiwa na Waargentina kuiongoza timu ya taifa ya Argentina kulinyakua kombe la dunia nchini Afrika Kusini.
Maradona alichaguliwa kuwa kocha wa Argentina mwaka 2008 baada ya kujiuzulu kwa kocha Alfio Basile.
Pamoja na Argentina kutoonyesha uwezo mkubwa katika mechi za hatua ya awali ya kufuzu fainali ya kombe hilo, hatimaye ilifanikiwa kupata tiketi ya kuja Afrika baadae mwaka huu.
Argentina ipo kundi moja na Nigeria pamoja Ugiriki na Korea Kusini.
source nifahamishe
Thursday, March 25, 2010
Messi Amuovateki Beckham Kwa Kuchukua Mshiko Mkubwa

David Beckham sio tena mcheza soka anayelipwa pesa nyingi kuliko wote kwani hivi sasa nyota wa Barcelona, Lionel Messi ndiye yupo kwenye chati anaingiza mshiko mkubwa zaidi kwa mwaka kuliko wachezaji wote duniani.
Lionel Messi nyota wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina ndiye mchezaji anayekamata mshiko mkubwa zaidi kwa mwaka kuliko wachezaji wote duniani.
Kwa mwaka, Messi anajiingizia kiasi paundi milioni 29.6 ambazo ni milioni 2.3 zaidi ya anazoingiza David Beckham.
Kwa mwaka Messi anapokea mshahara wa paundi milioni 9, analipwa bonasi ya paundi milioni 3.6 na anaingiza paundi milioni 17.1 kutokana na matangazo ya makamapuni mbali mbali kama vile adidas, Pepsi na Gillette.
Katika listi ya wachezaji 10 wanaojiingizia kipato kikubwa kwa mwaka, nyota wa Cameroon, Samuel Et'oo anashika nafasi ya 10 kwa kiasi chake cha paundi milioni 12.4.
Hata hivyo wachezaji wa soka bado hawajafanikiwa kuwaovateki kwa kipato wachezaji wa mpira wa kikapu na gofu.
Tiger Woods ndiye mwanamichezo anayeingiza mshiko mkubwa kuliko wanamichezo wote duniani, anayemfuatia ni mchezaji mwenzake wa gofu Phil Mickelson huku nyota wa mpira wa kikapu, LeBron James akishika nafasi ya tatu.
Orodha kamili ya wanasoka 10 wenye kipato kikubwa kwa mwaka ni kama ifuatavyo:
1. Lionel Messi (Barcelona) £29.6m
2. David Beckham (LA Galaxy) £27.3m
3. Cristiano Ronaldo (Real Madrid) £26.9m
4. Kaka (Real Madrid) £16.9m
5. Thierry Henry (Barcelona) £16.2m
6. Ronaldinho (AC Milan) £15.4m
7. Carlos Tevez (Manchester City) £13.8m
8. Zlatan Ibrahimovic (Barcelona) £13m
9. Frank Lampard (Chelsea) £12.7m
10. Samuel Eto’o (Inter Milan) £12.4m
source nifahamishe
Monday, March 22, 2010
Manchester United Yaikong'oli Liverpool 2-1

Manchester United imerudi tena kileleni mwa ligi ya Uingereza baada ya kufuta uteja wake kwa Liverpool kwa kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye uwanja wa Old Trafford jijini
VIDEO - Manchester United Yaikong'oli Liverpool 2-1
Wachezaji wa Manchester United wakipongezana Sunday, March 21, 2010 7:55 PM
Manchester United imerudi tena kileleni mwa ligi ya Uingereza baada ya kufuta uteja wake kwa Liverpool kwa kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye uwanja wa Old Trafford jijini Manchester. VIDEO za magoli yote katika mechi hii mwisho wa habari hii.
Matumaini ya Liverpool kutwaa nafasi ya nne katika msimamo wa ligi ya Uingereza ili kuweza kucheza kombe la mabingwa wa ulaya msimu ujao yamezidi kufifia baada ya kupoteza pointi zingine muhimu kwa Manchester United.
Liverpool iliingia uwanjani ikiwa na nia ya kuiharibia Manchester United kampeni yake ya kutwaa ubingwa wa Uingereza kwa mara 19 na hivyo kuivuka rekodi ya Liverpool ya mataji 18.
Iliwachukua dakika tano tu Liverpool kuweza kupata goli la kuongoza kupitia kwa Fernando Torres ambaye aliunganisha vyema krosi ya Dirk Kuyt na kumwacha kipa wa Manchester United, Edwin van der Sar aking'ang'aa macho.
Manchester United ilipewa penalti dakika tano baadae baada ya Javier Mascherano kumuangusha Antonio Valencia kwenye mstari wa 18. Wayne Rooney alipiga penalti hiyo ambayo iliokolewa na kipa wa Liverpool, Pepe Reina lakini mpira ulipomrudia tena Rooney hakufanya ajizi kuuzamisha nyavuni.
Jahazi la Liverpool lilizama kwenye dakika ya 15 ya kipindi cha pili wakati Park Ji-sung alipopiga mbizi na kuunganisha kwa kichwa krosi ya Gary Neville.
Goli hilo lilidumu hadi wakati refa wa mechi hiyo alipopuliza kipyenga cha kumaliza mpambano huo
source nifahamishe
Friday, March 19, 2010
Arsenal Kukumbana na Barcelona, Manchester na Bayern Munich

Heka heka za robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya zitaendelea tena wiki mbili zijazo kwa mabingwa watetezi Barcelona kupimana ubavu na Arsenal huku Manchester United ikitimua vumbi na Bayern Munich.
Ratiba ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya imetangazwa leo kwa timu ya Arsenal ya Uingereza kupangiwa mabingwa watetezi Barcelona ambao hivi sasa wanatisha kwa boli wanalolitandaza.
Manchester United itajaribu kukumbukia maajabu yake ya mwaka 1999 kwa kupimana ubavu na wababe wa bundesliga Bayern Munich.
Vijana wa Jose Mourinho, Inter Milan watatoana jasho na CSKA Moscow kuwania nafasi ya nusu fainali huku Lyon ya Ufaransa iliyoitupa nje ya mashindano Real Madrid, itakutana na ndugu zao Bordeaux.
Mechi za kwanza za robo fainali zitachezwa wiki mbili zijazo machi 30 na machi 31 huku mechi za marudiano zikipangwa kufanyika aprili 6 na 7.
Ratiba ya robo fainali inamfanya nyota wa Barcelona, Thierry Henry arudi uwanja wa Emirates kwa mara ya kwanza tangia alipouzwa kwa Barcelona mwaka 2007 kwa dau la paundi milioni 16.
Arsenal ambayo itacheza mechi ya kwanza nyumbani, itajaribu kulipa kisasi cha kichapo ilichopewa na Barcelona miaka minne iliyopita wakati ilipolazwa 2-1 na Barcelona kwenye mechi ya fainali wakati huo Thiery Henry akiichezea Arsenal.
Akizungumzia uwezo wa Barcelona kwa timu za Uingereza, Thiery Henry alisema kuwa Barcelona ipo kwenye chati ya juu sana hivi sasa na nyota wa Barcelona,Muargentina, Lionel Messi ndiye mtu atakayeharibu ndoto za timu za Uingereza kunyakua kombe la mabingwa wa ulaya.
source nifahamishe
Thursday, March 11, 2010
Didier Drogba ndio mwanasoka bora Afrika

Mchezaji matata wa Ivory Coast Didier Droga ameshinda tuzo la mwanasoka bora zaidi barani Afrika mwaka 2009.
Drogba alifunga mabao matano wakati Ivory Coast ilipofuzu kwa kombe la dunia na vile vile kuifungiaa klabu yake bao katika Mwenzake wa klabu hiyo Michael Essien na mchezaji wa Cameroon Samuel Eto'o waliteuliwa kuwania tuzo hiyo.
Drogba, aliyefikisha umri wa miaka 32, hapo jana, amewahi kushinda tuzo hiyo mwaka wa 2006.
Timu ya taifa ya Algeria ilitajwa kuwa timu bora zaidi mwaka huu katika sherehe iliyofanyika mjini Accra, Ghana. ya kombe la FA...
source gblp
Wednesday, February 24, 2010
Inter Milan Yaibanjua Chelsea 2-1

Jose Mourinho ameiongoza vyema timu yake ya Inter Milan kuibanjua timu yake ya zamani Chelsea ya Uingereza kwa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza ya mtoano ya kombe la mabingwa wa ulaya.
Timu ya Chelsea ya Uingereza imekumbana na kichapo kwenye uwanja wa San Siro jijini Milan kwenye mechi ya kwanza ya mtoano dhidi ya Inter Milan ya Italia ambayo hivi sasa inafundishwa na Jose Mourinho ambaye zamani aliwahi kuwa kocha wa Chelsea.
Inter walifanikiwa kuliona lango la Chelsea mapema kwenye dakika ya tatu ya mchezo kupitia kwa Diego Milito.
Chelsea walijipanga vyema baada ya bao hilo na kuanza kulisakama lango la Inter lakini juhudi zao zilizaa matunda kwenye kipindi cha pili pale Solomon Kalou alipoipatia Chelsea goli la kusawazisha.
Hata hivyo furaha za wapenzi wa Chelsea hazikudumu dakika nyingi kwani Esteban Cambiasso alifanikiwa kuipatia Inter goli la pili na la ushindi kwenye mechi hiyo.
Timu hizo zitarudiana tena kwenye uwanja wa Stamford Bridge jijini London baada ya wiki tatu.
source nifahamishe
Subscribe to:
Posts (Atom)
