Sunday, April 3, 2011

Jambazi 'Obama' Atiwa Mbaroni



Polisi wa nchini Austria wamemtia mbaroni mwanaume mmoja wa nchini humo ambaye alikuwa akifanya matukio ya uporaji pesa kwenye mabenki akiwa amevaa kinyago chenye sura ya rais wa Marekani, Barack Obama.
Taarifa ya polisi wa Vienna, Austria imesema kuwa mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 45 raia wa Ujerumani anatuhumiwa kupora pesa kwenye benki zipatazo 7 za nchini humo ambapo wakati wote alikuwa akivaa kinyago chenye sura ya Barack Obama.

Polisi walisema kuwa tangu mwaka 2008, mwanaume huyo alifanya matukio 7 ya uporaji pesa kwenye mabenki na tukio lake la mwisho la uhalifu alilifanya mchana wa siku ya alhamisi katika kijiji cha Fornach.

Msako wa polisi ulianza na alitiwa mbaroni muda mfupi baadae baada ya mbwa wa polisi kufanikiwa kukiona kinyago na silaha alizokuwa akizitumia jambazi huyo.

Jambazi huyo alikiri kufanya matukio ya ujambazi na polisi walitangaza kuwa wana furaha wamemtia mbaroni jambazi waliyekuwa wakimtafuta kwa muda mrefu.


source nifahamishe

Thursday, June 10, 2010

Benitez ahamia inter..........


baada ya kutemwa liverpool sasa atapa dau kwa inter ameshafanya mkataba wa miaka 2.

Friday, June 4, 2010

Liverpool Yamtema Benitez


Baada ya Liverpool kuvurunda msimu uliopita na kumaliza ligi ikiwa imeshika nafasi ya saba, kocha wa Liverpool Rafa Benitez amepoteza kazi yake baada ya miaka sita ya kuiongoza Liverpool.
Rafa Benitez ametemwa na Liverpool baada ya miaka sita kufuatia kufanya vibaya kwa Liverpool katika msimu uliopita.

Liverpool ilimaliza ligi ikishika nafasi ya saba, ilitolewa mapema kwenye makombe ya Carling na kombe la FA, haikufika kokote kwenye kombe la mabingwa wa ulaya kabla ya kutolewa nusu fainali kwenye kombe la UEFA.

Liverpool imemlazimisha Benitez achukue mikoba yake kwa kukatisha mkataba wake na kumlipa fidia ambayo inakadiriwa kufikia paundi milioni sita.

Benitez mwenye umri wa miaka 50 alisema baada ya kujulishwa kuwa kibarua chake kimeota mbawa: "Nina huzuni sana kutangaza kuwa sitaendelea kuwa kocha wa Liverpool FC. Napenda kuwashukuru wafanyakazi wote na wachezaji kwa juhudi zao".

Mwenyekiti wa Liverpool, Martin Broughton aliongeza: "Rafa ataendelea kukumbukwa na Liverpool kwa kutuletea kombe la mabingwa wa ulaya katika fainali dhidi ya AC Milan mjini Istanbul".

Broughton aliongeza kuwa baada ya msimu ambao haukuwa na matokeo mazuri, Liverpool imeona ni bora ijijenge tena upya.

Mchakato wa kutafuta kocha mpya wa Liverpool umeanza.

source nifahamishe

Monday, May 31, 2010

Eto'o Atishia Kuitosa Cameroon Baada ya Kukosolewa na Roger Milla


Nyota wa timu ya taifa ya Cameroon, Samuel Eto'o ametishia kujitoa kwenye timu ya Cameroon itakayoshiriki kombe la dunia baada ya kukosolewa na mkongwe wa soka Afrika, Roger Milla.
Mshambuliaji wa Inter Milan Samuel Eto'o ametishia kususia kuichezea Cameroon baada ya kukosolewa na nyota wa Cameroon wa kombe la dunia la 1990, Roger Milla kuwa hajitumi anapoichezea timu ya taifa.

Akiongea hivi karibuni na vyombo vya habari, Roger Milla alimkosoa Eto'o akisema kuwa Eto'o hujituma zaidi anapoichezea yake ya Inter Milan kuliko anapoichezea timu yake ya taifa.

Akiongea na televisheni ya Canal Plus Sport ya Ufaransa, Eto'o alielezea kukasirishwa na maoni ya Roger Milla na kuongeza kuwa huenda akajitoa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon kitakachoshiriki fainali za kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

"Kwani kombe la dunia ndio la muhimu sana kwangu?", alisema Eto'o.

"Bado nina siku chache za kufikiria nichukue uamuzi gani kwakuwa huwa sipendi mambo kama haya", aliongeza Eto'o.

"Roger Milla amefanya nini cha maana? amewahi kuchukua kombe la dunia? timu yake ya mwaka 1990 iliishia robo fainali", alisema Eto'o kwa hasira.

Hata hivyo pamoja na Eto'o kutishia kuitosa Cameroon, kocha wa Cameroon, Paul Le Guen alimtaja Eto'o kwenye kikosi chake cha wachezaji 23 kitakachoenda Afrika Kusini kwenye fainali za kombe la dunia.

Kikosi kamili cha Cameroon ni kama ifuatavyo:

Hamidou Souleymanou (Kayserispor), Carlos Kameni (Espanyol), Guy Roland Ndy Assembe (Valenciennes); Benoit Assou-Ekotto (Tottenham), Sebastien Bassong (Tottenham), Gaetan Bong (Valenciennes), Aurelien Chedjou (Lille), Geremi (Ankaragucu), Stephane Mbia (Marseille), Nicolas Nkoulou (Monaco), Rigobert Song (Trabzonspor); Eyong Enoh (Ajax), Jean II Makoun (Lyon), Georges Mandjeck (Kaiserslautern), Joel Matip (Schalke), , Landry Nguemo (Celtic), Alexandre Song (Arsenal); Vincent Aboubakar (Coton Sport), Eric Choupo-Moting (Nuremberg), Achille Emana (Betis), Samuel Eto'o (Inter Milan), Mohamadou Idrissou (Freiburg), Achille Webo (Mallorca).

source nifahamishe

Friday, May 28, 2010

Jose Mourinho Atua Real Madrid


Wababe wa Hispania Real Madrid, wamefanikiwa kumnyakua kocha wa mabingwa wa ulaya Inter Milan ya Italia, Jose Mourinho.
Baada ya kutwaa makombe matatu msimu huu, kocha wa Inter Milan, Jose Mourinho ameitosa timu hiyo na kuhamia kwa timu tajiri duniani ya Real Madrid ya Hispania.

Tovuti ya Real Madrid ilitoa taarifa leo kuwa makubaliano yamefikiwa kati ya Inter Milan na Real Madrid hivyo Mourinho ndiye atakayekuwa kocha mpya wa Real Madrid.

Awali kabla ya makubaliano hayo kufikiwa, Inter Milan iligoma kumuachia Mourinho ikitaka ilipwe fidia ya euro milioni 16 kwa Mourinho kukatisha mkataba wake ambao umebakiza miaka miwili.

Rais wa Real Madrid Florentino Perez alienda Milan kukutana na mwenyekiti wa Inter Milan Massimo Moratti ili kufikia muafaka juu ya suala hilo la Mourinho. hata hivyo maafikiano yaliyofikiwa na klabu hizo hayakuwekwa wazi.

Jose Mourinho atatambulishwa kwa wapenzi wa Real Madrid siku ya jumatatu saa saba mchana kwa saa za Tz kwenye uwanja wa Real Madrid wa Santiago Bernabeu.

source nifahamishe

Sunday, May 23, 2010

Inter Milan Ndio Mabingwa wa Ulaya, Yaibanjua Bayern 2-0


Kocha wa Inter Milan ya Italia Jose Mourinho akiingiza uwanjani kikosi ambacho hakikuwa na Muitaliano hata mmoja, amedhihirisha makali yake mbele ya bosi wake wa zamani kocha wa Bayern Munich, Louis van Gaal kwa kuigaragaza Bayern kwa mabao 2-0.
Internazionale Milano (Inter Milan) imekuwa mabingwa wapya wa ulaya baada ya kuwatungua Bayern Munich kwa magoli 2-0 katika mchezo wa fainali ya mabingwa wa ulaya iliyochezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu.

Inter Milan imechukua kombe leo ikiwa ni miaka 45 tangia ilipochukua mara ya mwisho kombe barani ulaya. Wakati huo kocha wake Jose Mourinho alikuwa na umri wa miaka miwili. Leo Mourinho akiwa na umri wa miaka 47 ameiwezesha Inter Milan kurudi katika anga la soka la ulaya na kuwa mabingwa wapya wa ulaya.

Ingawa Inter Milan ni timu ya Italia lakini kocha wa Inter Milan Jose Mourinho hakumuingiza mchezaji hata mmoja toka Italia katika kikosi chake cha kwanza. Muitaliano pekee aliyecheza mechi ya leo alikuwa ni Marco Materazzi ambaye aliingia uwanjani dakika mbili kabla ya mechi kuisha.

Bayern Munich ingawa ilitawala mechi yote na kumiliki mpira muda mrefu walishindwa kuivunja ngome ya Inter Milan ambayo ilicheza kwa kujilinda zaidi staili ambayo Mourinho hupenda kuitumia anapokuwa katika wakati mgumu.

Magoli mawili ya Muargentina Diego Milito katika dakika ya 35 na 70 yaliiwezesha Inter Milan kuwa mabingwa wapya wa ulaya kwa msimu wa mwaka 2009-2010.

Jose Mourinho ambaye kuna uwezekano mkubwa akaikimbia Inter Milan msimu ujao kwenda kuifundisha Real Madrid, amemaliza msimu huu kwa kuiwezesha Inter Milan kutwaa jumla ya makombe matatu.

source nifahamishe

Sunday, May 16, 2010

Chelsea Yaibanjua Portsmouth na Kutwaa Kombe la FA


Mabingwa wa ligi ya Uingereza, Chelsea wameongeza kombe jingine kwenye hazina yake mwaka huu baada ya kuwabanjua Portsmouth kwa goli 1-0 kwenye fainali ya kombe la FA.
Goli lililofungwa na nyota wa mchezo Didier Drogba kwa mkwaju wa adhabu ndogo, liliiwezesha Chelsea kutwaa makombe mawili katika msimu mmoja kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Kocha wa Chelsea ambaye alianza kuifundisha Chelsea mwanzoni mwa msimu ulioisha amemaliza msimu wake wa kwanza Uingereza akiwa amejikusanyia makombe matatu, kombe la ngao, kombe la ligi ya Uingereza na kombe la FA.

Katika mechi ya leo, Chelsea haikupata ushindi kirahisi kwani Portsmouth mbali ya kushuka daraja ilitandaza soka safi na kumweka kipa wa Chelsea, Petr Cech kwenye heka heka mara kwa mara.

Cech aliwanyima Portsmouth goli ambalo lingebadilisha muelekeo wa mchezo kwenye dakika ya 56, alipoipangua penalti iliyopigwa na nyota wa Portsmouth, Kevin Prince Boateng.

Kipa wa Portsmouth, David James ndiye aliyekuwa kwenye patashika muda wote kutokana na mashambulizi makali ya Chelsea yaliyoongozwa na Drogba.

Katika kipindi cha kwanza pekee, Chelsea waliwakosakosa Portsmouth ambapo mara tano mpira uligonga mwamba na kugoma kuingia nyavuni.

Kombe la leo limekuwa kombe la nane la nahodha wa Chelsea, John Terry tangu alipoanza kuichezea timu hiyo.

source nifahamishe