Monday, May 31, 2010

Eto'o Atishia Kuitosa Cameroon Baada ya Kukosolewa na Roger Milla


Nyota wa timu ya taifa ya Cameroon, Samuel Eto'o ametishia kujitoa kwenye timu ya Cameroon itakayoshiriki kombe la dunia baada ya kukosolewa na mkongwe wa soka Afrika, Roger Milla.
Mshambuliaji wa Inter Milan Samuel Eto'o ametishia kususia kuichezea Cameroon baada ya kukosolewa na nyota wa Cameroon wa kombe la dunia la 1990, Roger Milla kuwa hajitumi anapoichezea timu ya taifa.

Akiongea hivi karibuni na vyombo vya habari, Roger Milla alimkosoa Eto'o akisema kuwa Eto'o hujituma zaidi anapoichezea yake ya Inter Milan kuliko anapoichezea timu yake ya taifa.

Akiongea na televisheni ya Canal Plus Sport ya Ufaransa, Eto'o alielezea kukasirishwa na maoni ya Roger Milla na kuongeza kuwa huenda akajitoa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon kitakachoshiriki fainali za kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

"Kwani kombe la dunia ndio la muhimu sana kwangu?", alisema Eto'o.

"Bado nina siku chache za kufikiria nichukue uamuzi gani kwakuwa huwa sipendi mambo kama haya", aliongeza Eto'o.

"Roger Milla amefanya nini cha maana? amewahi kuchukua kombe la dunia? timu yake ya mwaka 1990 iliishia robo fainali", alisema Eto'o kwa hasira.

Hata hivyo pamoja na Eto'o kutishia kuitosa Cameroon, kocha wa Cameroon, Paul Le Guen alimtaja Eto'o kwenye kikosi chake cha wachezaji 23 kitakachoenda Afrika Kusini kwenye fainali za kombe la dunia.

Kikosi kamili cha Cameroon ni kama ifuatavyo:

Hamidou Souleymanou (Kayserispor), Carlos Kameni (Espanyol), Guy Roland Ndy Assembe (Valenciennes); Benoit Assou-Ekotto (Tottenham), Sebastien Bassong (Tottenham), Gaetan Bong (Valenciennes), Aurelien Chedjou (Lille), Geremi (Ankaragucu), Stephane Mbia (Marseille), Nicolas Nkoulou (Monaco), Rigobert Song (Trabzonspor); Eyong Enoh (Ajax), Jean II Makoun (Lyon), Georges Mandjeck (Kaiserslautern), Joel Matip (Schalke), , Landry Nguemo (Celtic), Alexandre Song (Arsenal); Vincent Aboubakar (Coton Sport), Eric Choupo-Moting (Nuremberg), Achille Emana (Betis), Samuel Eto'o (Inter Milan), Mohamadou Idrissou (Freiburg), Achille Webo (Mallorca).

source nifahamishe

Friday, May 28, 2010

Jose Mourinho Atua Real Madrid


Wababe wa Hispania Real Madrid, wamefanikiwa kumnyakua kocha wa mabingwa wa ulaya Inter Milan ya Italia, Jose Mourinho.
Baada ya kutwaa makombe matatu msimu huu, kocha wa Inter Milan, Jose Mourinho ameitosa timu hiyo na kuhamia kwa timu tajiri duniani ya Real Madrid ya Hispania.

Tovuti ya Real Madrid ilitoa taarifa leo kuwa makubaliano yamefikiwa kati ya Inter Milan na Real Madrid hivyo Mourinho ndiye atakayekuwa kocha mpya wa Real Madrid.

Awali kabla ya makubaliano hayo kufikiwa, Inter Milan iligoma kumuachia Mourinho ikitaka ilipwe fidia ya euro milioni 16 kwa Mourinho kukatisha mkataba wake ambao umebakiza miaka miwili.

Rais wa Real Madrid Florentino Perez alienda Milan kukutana na mwenyekiti wa Inter Milan Massimo Moratti ili kufikia muafaka juu ya suala hilo la Mourinho. hata hivyo maafikiano yaliyofikiwa na klabu hizo hayakuwekwa wazi.

Jose Mourinho atatambulishwa kwa wapenzi wa Real Madrid siku ya jumatatu saa saba mchana kwa saa za Tz kwenye uwanja wa Real Madrid wa Santiago Bernabeu.

source nifahamishe

Sunday, May 23, 2010

Inter Milan Ndio Mabingwa wa Ulaya, Yaibanjua Bayern 2-0


Kocha wa Inter Milan ya Italia Jose Mourinho akiingiza uwanjani kikosi ambacho hakikuwa na Muitaliano hata mmoja, amedhihirisha makali yake mbele ya bosi wake wa zamani kocha wa Bayern Munich, Louis van Gaal kwa kuigaragaza Bayern kwa mabao 2-0.
Internazionale Milano (Inter Milan) imekuwa mabingwa wapya wa ulaya baada ya kuwatungua Bayern Munich kwa magoli 2-0 katika mchezo wa fainali ya mabingwa wa ulaya iliyochezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu.

Inter Milan imechukua kombe leo ikiwa ni miaka 45 tangia ilipochukua mara ya mwisho kombe barani ulaya. Wakati huo kocha wake Jose Mourinho alikuwa na umri wa miaka miwili. Leo Mourinho akiwa na umri wa miaka 47 ameiwezesha Inter Milan kurudi katika anga la soka la ulaya na kuwa mabingwa wapya wa ulaya.

Ingawa Inter Milan ni timu ya Italia lakini kocha wa Inter Milan Jose Mourinho hakumuingiza mchezaji hata mmoja toka Italia katika kikosi chake cha kwanza. Muitaliano pekee aliyecheza mechi ya leo alikuwa ni Marco Materazzi ambaye aliingia uwanjani dakika mbili kabla ya mechi kuisha.

Bayern Munich ingawa ilitawala mechi yote na kumiliki mpira muda mrefu walishindwa kuivunja ngome ya Inter Milan ambayo ilicheza kwa kujilinda zaidi staili ambayo Mourinho hupenda kuitumia anapokuwa katika wakati mgumu.

Magoli mawili ya Muargentina Diego Milito katika dakika ya 35 na 70 yaliiwezesha Inter Milan kuwa mabingwa wapya wa ulaya kwa msimu wa mwaka 2009-2010.

Jose Mourinho ambaye kuna uwezekano mkubwa akaikimbia Inter Milan msimu ujao kwenda kuifundisha Real Madrid, amemaliza msimu huu kwa kuiwezesha Inter Milan kutwaa jumla ya makombe matatu.

source nifahamishe

Sunday, May 16, 2010

Chelsea Yaibanjua Portsmouth na Kutwaa Kombe la FA


Mabingwa wa ligi ya Uingereza, Chelsea wameongeza kombe jingine kwenye hazina yake mwaka huu baada ya kuwabanjua Portsmouth kwa goli 1-0 kwenye fainali ya kombe la FA.
Goli lililofungwa na nyota wa mchezo Didier Drogba kwa mkwaju wa adhabu ndogo, liliiwezesha Chelsea kutwaa makombe mawili katika msimu mmoja kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Kocha wa Chelsea ambaye alianza kuifundisha Chelsea mwanzoni mwa msimu ulioisha amemaliza msimu wake wa kwanza Uingereza akiwa amejikusanyia makombe matatu, kombe la ngao, kombe la ligi ya Uingereza na kombe la FA.

Katika mechi ya leo, Chelsea haikupata ushindi kirahisi kwani Portsmouth mbali ya kushuka daraja ilitandaza soka safi na kumweka kipa wa Chelsea, Petr Cech kwenye heka heka mara kwa mara.

Cech aliwanyima Portsmouth goli ambalo lingebadilisha muelekeo wa mchezo kwenye dakika ya 56, alipoipangua penalti iliyopigwa na nyota wa Portsmouth, Kevin Prince Boateng.

Kipa wa Portsmouth, David James ndiye aliyekuwa kwenye patashika muda wote kutokana na mashambulizi makali ya Chelsea yaliyoongozwa na Drogba.

Katika kipindi cha kwanza pekee, Chelsea waliwakosakosa Portsmouth ambapo mara tano mpira uligonga mwamba na kugoma kuingia nyavuni.

Kombe la leo limekuwa kombe la nane la nahodha wa Chelsea, John Terry tangu alipoanza kuichezea timu hiyo.

source nifahamishe

Tuesday, May 11, 2010

Nigeria Yatangaza Kikosi cha Kombe la Dunia


Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles ametangaza kikosi cha wachezaji watakaoiwakilisha Nigeria kwenye kombe la dunia mwezi ujao nchini Afrika Kusini bila ya kumsahau mtu mzima Nwanko Kanu.
Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria Lars Lagerback ambaye alikabidhiwa mikoba ya ukocha wa Nigeria baada ya kocha Shaibu Amodu kuvurunda kwenye fainali za kombe la mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Angola, ametangaza kikosi cha awali cha wachezaji 30 ambacho baadae kitachujwa na kubaki na wachezaji 23 watakoiwakilisha Nigeria kwenye fainali za kombe la dunia zinazoanza mwezi ujao.

Katika kikosi hicho Lars amemuita nyota wa Portsmouth ya Uingereza iliyoshuka daraja, mkongwe Nwanko Kanu.

Magolikipa watatu kati ya wanne walioitwa na kocha wa Nigeria wanacheza soka nchini Israel.

Kikosi kamili cha Nigeria ni kama ifuatavyo:

Magolikipa: Vincent Enyeama (Hapoel Tel Aviv, Israel), Dele Aiyenugba (Bnei Yehuda, Israel), Austin Ejide (Hapoel Petah Tikva, Israel), Bassey Akpan (Bayelsa United, Nigeria)

Mabeki: Taye Taiwo (Marseille, France), Elderson Echiejile (Rennes, France), Chidi Odiah (CSKA Moscow, Russia), Onyekachi Apam (OG Nice, France), Joseph Yobo (Everton, England), Daniel Shittu (Bolton Wanderers, England), Ayodele Adeleye (Sparta Rotterdam, Netherlands), Rabiu Afolabi (SV Salzburg, Austria), Terna Suswan (Lobi Stars, Nigeria)

Viungo: Chinedu Ogbuke Obasi (TSG Hoffenheim, Germany), John Utaka (Portsmouth, England), Brown Ideye (FC Sochaux, France), Peter Utaka (Odense Boldklub, Denmark), Kalu Uche (Almeria, Spain), Dickson Etuhu (Fulham, England), John Mikel Obi (Chelsea, England), Sani Kaita (Alaniya, Russia), Haruna Lukman (AS Monaco, France), Yusuf Ayila (Dynamo Kiev, Ukraine), Osaze Odemwingie (Lokomotiv Moscow, Russia)

Washambuliaji: Yakubu Aiyegbeni (Everton, England), Victor Anichebe (Everton, England), Nwankwo Kanu (Portsmouth, England), Obafemi Martins (Wolfsburg, Germany), Ikechukwu Uche (Real Zaragoza, Spain), Victor Obinna Nsofor (Malaga, Spain)


source nifahamishe

Monday, May 10, 2010

Chelsea Ndio Mabingwa wa Uingereza


Wazee wa darajani Chelsea wamekatisha matumaini ya Manchester United kutwaa ubingwa wa Uingereza kwa mara ya nne mfululizo baada ya kuunyakua ubingwa wa Uingereza kwa kutoa kipigo cha nguvu kwa Wigan kwa kuiburuza magoli 8-0.
Magoli manane waliyobugizwa Wigan Athletic leo kwenye uwanja wa Stamford Bridge yameiwezesha timu ya Chelsea kutwaa tena kombe la ubingwa wa ligi ya Uingereza kwa mara ya nne katika historia ya timu hiyo.

Ushindi wa magoli 4-0 ilioupata Manchester United dhidi ya Stoke City haukuweza kuwasaidia kunyakua taji la ligi ya Uingereza kwa mara ya 19.

Magoli matatu ya Didier Drogba kwenye kipindi cha pili yalimwezesha kuwa mfungaji bora wa ligi ya Uingereza kwa msimu wa mwaka 2009/2010.

Magoli mengine ya Chelsea katika ushindi wa leo yalifungwa na Nicolas Anelka, Salomon Kalou, Ashley Cole na Frank Lampard.

Kocha wa Chelsea amekuwa miongoni mwa makocha wachache sana katika ligi ya Uingereza ambao walifanikiwa kutwaa ubingwa katika mwaka wao wa kwanza wa kuanza kazi.

Chelsea sasa ina mpango wa kuongeza kombe jingine kwenye hazina yake mwaka huu wakati itakapopimana ubavu na Portsmouth kwenye mechi ya fainali ya kombe la FA itakayochezwa jumamosi ijayo kwenye uwanja wa Wembley.


source nifahamishe

Messi Kuvunja rekodi Ya Dunia Usajili Msimu Ujao


Nyota wa Argentina na timu ya Barcelona ya Hispania, Lionel Messi anatabiriwa kuvunja rekodi ya dunia ya usajili msimu ujao kwa jinsi timu tajiri za barani ulaya zinavyojiandaa kutoa donge nene kwa Barcelona ili kuwashawishi wamuuze nyota wao huyo.
Vyanzo mbalimbali vya habari vimeanza kumtabiria nyota wa klabu ya Barcelona Lionel Messi kuvunja rekodi ya dunia ya usajili pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa katika msimu ujao.

Habari zinasema tayari klabu mbalimbali za ulaya zimeanza mikakati ya kuitafuta saini ya messi huku nyingine zikianza kupiga hodi Barca zikiishawiwishi klabu hiyo kumuachia messi kwa gharama kubwa.

Miongoni mwa klabu ambazo zimeonyesha nia ya kutaka kuvunja akaunti yao benki ni Real Madrid matajiri wa hispania ambapo tayari wameshatangaza dau la kitita cha paundi miloni 120 kumng’oa nyota huyo Barcelona na kumuingiza Santiago Bernabeu.

Madrid ambayo msimu uliopita ilivunja rekodi ya dunia katika usajili wa mchezaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo ikilipa paundi milioni 80 sasa imedhamiria kuvunja rekodi nyingine kwa mchezaji huyo wa kimataifa Lionel Messi.

Mpango halisi wa Madrid ni kumngo’oa Messi kwa mkataba wa paundi milioni 120 ambapo unaonekana kuanza kufanyiwa kazi na maafisa wa klabu hiyo.

Lakini mpango huo umekuwa ukichukuliwa kwa hisia tofauti na klabu hiyo ya Barcelona ambapo inasemekana bado uongozi unajadili kuchukua fedha na kuuvunja mwamba au kuacha fedha na kuboresha ngome yao katika msimu ujao.


source nifahamishe