Monday, April 19, 2010

Skendo la Ngono Laikumba Timu ya Taifa ya Ufaransa


Skendo kubwa la ngono limeikumba timu ya taifa ya soka ya Ufaransa ambapo baadhi ya nyota wa timu hiyo ya taifa wanadaiwa kufanya mapenzi na machangudoa wenye umri mdogo.
Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya soka ya Ufaransa wamehusishwa kwenye skendo la kufanya mapenzi na makahaba wenye umri chini ya miaka 18.

Mchezaji nyota wa Ufaransa, Franck Riberry na Sidney Govou ni wachezaji wawili waliotajwa ambao tayari wameishahojiwa na polisi kuhusiana na skendo hilo.

Riberry anayeichezea Bayern Munich ya Ujerumani ana mke lakini naye amenaswa katika skendo hilo akidaiwa kufanya mapenzi na msichana kahaba mwenye umri chini ya miaka 18.

Taarifa zilisema kuwa wachezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa "Les Bleus" walikuwa wakienda sana kwenye klabu moja ya starehe ya jijini Paris ambapo walikuwa wakiandaliwa makahaba wenye umri chini ya miaka 18. Mmoja wa makahaba hao inadaiwa alikuwa na umri wa miaka 14.

Wachezaji wengine nyota wa Ufaransa nao wamehusishwa na skendo hilo lakini majina yao yamewekwa kapuni.

Mmoja wa wachezaji hao alikiri kufanya mapenzi na msichana mwenye umri mdogo lakini alijitetea kuwa wakati huo alikuwa akiamini kuwa mwanamke aliyeletewa ni mtu mzima.

Kuwadi "Pimp" anayedaiwa kuwaandalia wachezaji machangudoa hao ametiwa mbaroni na baadhi ya wasichana hao wanaendelea kuhojiwa na polisi.

Skendo hilo limekuja ikiwa ni miezi miwili tu kabla ya Ufaransa kuja barani Afrika kwaajili ya fainali za kombe la dunia.


source nifahamishe

No comments:

Post a Comment