Sunday, April 18, 2010

Tottenham Yaharibu Sherehe za Chelsea

Tottenham Hostspur ya jijini London imevuruga mahesabu ya wazee wa darajani Chelsea kutwaa ubingwa wa ligi ya Uingereza kwa kuizamisha kwa mabao 2-1 huku Manchester United ikiwazamisha watani wake wa jadi Manchester City kwa bao 1-0.
Vinara wa ligi ya Uingereza Chelsea leo wamepigwa mwereka na Tottenham Hotspur na kuzamishwa mabao 2-1 na hivyo kuyafanya matumaini ya Chelsea kutwaa ubingwa wa Uingereza mapema kuyeyuka.

Kabla ya mechi Chelsea ilikuwa ikiongoza ligi ya Uingereza kwa tofautiya pointi nne na Manchester United lakini kipigo cha Chelsea na kushinda kwa Manchester United dhidi ya watani wao wa jadi Manchester City kumelifanya pengo la pointi kati ya Chelsea na Manchester United kupungua hadi pointi moja.

Chelsea imebakiza mechi tatu dhidi ya Stoke City, Liverpool na Wigan na italazimika kushinda mechi zote ili kujihakikishia ubingwa.

Kwa upande wake, Manchester United imebakiza mechi tatu dhidi ya Tottenham, Sunderland na Stoke City.

source nifahamishe

No comments:

Post a Comment