Wednesday, March 31, 2010

Arsenal Chupu Chupu Kuzamishwa na Barcelona


Arsenal imenusurika chupu chupu kupokea kichapo toka kwa Barcelona na kuzalimisha sare ya bao 2-2 kwenye uwanja wake wa Emirates. Katika mechi nyingine ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya, Inter Barcelona ikitandaza soka ambalo liliwafanya wenyeji Arsenal waonekane kama wageni kwenye uwanja wao wa Emirates, ilishindwa kuyalinda magoli yake mawili na kukubali kutoka sare ya bao 2-2 na vijana wa Arsene Wenger.

Hata hivyo Barcelona bado inapewa nafasi kubwa ya kusonga mbele katika mechi ya marudiano jumanne ijayo kutokana na faida ya magoli mawili ya ugenini na kuumia kwa wachezaji watatu tegemezi wa Arsenal, Cesc Fabregas, William Gallas na Andrey Arshavin.

Barcelona ilianza kwa kasi kubwa sana mechi hiyo na kuifanya Arsenal itumie muda mwingi ndani ya nusu ya uwanja wake kulilinda lango lake.

Kipa wa Arsenal, Manuel Almunia alikuwa mkombozi wa Arsenal kwenye kipindi cha kwanza kutokana na jinsi alivyookoa mashambulizi makali ya Barcelona.

Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa sare ya bila kufungana.

Kipindi cha pili kilianza kwa Zlatan Ibrahimovic kuiandikia Barcelona goli la kwanza sekunde chache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili. Ibrahimovic aliongeza goli la pili kwenye dakika ya 59.

Kuingia kwa Theo Walcott kwenye dakika 65 ya kuliongeza kasi ya mashambulizi ya Arsenal na alikuwa ni Walcott aliyeipatia Arsenal goli la kwanza dakika 69.

Kwenye dakika ya 85, nahodha wa Barcelona, Puyol alimkwatua Fabregas ndani ya 18 na kupelekea penalti ambayo iliwekwa kimiani na Fabregas mwenyewe kabla hajatoka nje ya uwanja akichechemea.

Arsenal sasa italazimika kuifunga Barcelona au kutoka sare ya mabao zaidi ya mawili ili kuweza kusonga mbele.

Katika mechi nyingine ya robo fainali ya kombe la mabingwa wa ulaya, Inter Milan iliibanjua CSKA Moscow 1-0 kwenye uwanja wa San Siro.
iliifunga CSKA Moscow 1-0.

source nifahamishe

No comments:

Post a Comment