Monday, May 10, 2010

Messi Kuvunja rekodi Ya Dunia Usajili Msimu Ujao


Nyota wa Argentina na timu ya Barcelona ya Hispania, Lionel Messi anatabiriwa kuvunja rekodi ya dunia ya usajili msimu ujao kwa jinsi timu tajiri za barani ulaya zinavyojiandaa kutoa donge nene kwa Barcelona ili kuwashawishi wamuuze nyota wao huyo.
Vyanzo mbalimbali vya habari vimeanza kumtabiria nyota wa klabu ya Barcelona Lionel Messi kuvunja rekodi ya dunia ya usajili pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa katika msimu ujao.

Habari zinasema tayari klabu mbalimbali za ulaya zimeanza mikakati ya kuitafuta saini ya messi huku nyingine zikianza kupiga hodi Barca zikiishawiwishi klabu hiyo kumuachia messi kwa gharama kubwa.

Miongoni mwa klabu ambazo zimeonyesha nia ya kutaka kuvunja akaunti yao benki ni Real Madrid matajiri wa hispania ambapo tayari wameshatangaza dau la kitita cha paundi miloni 120 kumng’oa nyota huyo Barcelona na kumuingiza Santiago Bernabeu.

Madrid ambayo msimu uliopita ilivunja rekodi ya dunia katika usajili wa mchezaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo ikilipa paundi milioni 80 sasa imedhamiria kuvunja rekodi nyingine kwa mchezaji huyo wa kimataifa Lionel Messi.

Mpango halisi wa Madrid ni kumngo’oa Messi kwa mkataba wa paundi milioni 120 ambapo unaonekana kuanza kufanyiwa kazi na maafisa wa klabu hiyo.

Lakini mpango huo umekuwa ukichukuliwa kwa hisia tofauti na klabu hiyo ya Barcelona ambapo inasemekana bado uongozi unajadili kuchukua fedha na kuuvunja mwamba au kuacha fedha na kuboresha ngome yao katika msimu ujao.


source nifahamishe

No comments:

Post a Comment