Tuesday, February 16, 2010

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Wanawake Chatangazwa


Kikosi cha timu ya taifa ya wanawake ya Twiga Stars kitakachoshiriki michuano ya awali ya kufuzu kushiriki fainali za Afrika kwa upande wa wanawake nchini Afrika Kusini kimetangazwa.
Adolf Rishard, Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya wanawake ya Twiga Stars itakayoshiriki katika michuano ya awali ya kufuzu kushiriki fainali za Afrika za wanawake nchini Afrika Kusini, ametangaza kikosi cha wachezaji 27 kitakachopambana na timu ya taifa Ethiopia.

Mechi hiyo itachezwa Machi 6 mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Adolf alitangaza majina hayo kwa niaba ya kocha mkuu Charles Boniface ambaye yupo nje ya jiji la Dar es Salaam.

Wachezaji hao tayari wameingia kambini jana katika Hosteli ya Lamada iliyopo Ilala jiji Dar es Salaam.

Adolf akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za Chama cha Mpira wa miguu nchini TFF alisema kuwa yeye kwa uhakika haifahamu timu ya Ethiopia lakini anacho jua ni timu nzuri na watahakikisha yeye na kocha wake mkuu wanafanya kila liwezekanalo katika kuwaandaa vijana wao Twiga stars wanaoendelea na mazoezi katika Uwanja wa Karume uliopo katika ofisi za TFF.

Aliwataja wachezaji watakaoiwakilisha Tanzania kuwa ni Fatma Omari ,Pulkeria Chalaji, Sofia Mwasikila, Mary Masatu, Estar Chabuluma, Fatuma Mstafa, Zena Juma na Fatuma Bushiri.

Wengine ni pamoja na Neema Kuga, Hindu Muharami, Aisha Rashidi, Fadhila Kilele, Mwanahamisi Omary, Fatuma Hatibu, Mwanaidi Temba, Zena Hamisi na Hellen Peter.

Katika orodha hiyo pia wamo Pridian Daud Ettoo Mlezi, Fadhia Hamadi, Maimuna Said, Nasiria Ashri Abdallah, Mwajuma Abdalaah, Hakima Mwasilimu Hamis ,Warda Khalid Abdallah, Musimu Suluhu Hussan na Anita Elias.

source nifahamishe

No comments:

Post a Comment