Wednesday, February 24, 2010

Inter Milan Yaibanjua Chelsea 2-1


Jose Mourinho ameiongoza vyema timu yake ya Inter Milan kuibanjua timu yake ya zamani Chelsea ya Uingereza kwa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza ya mtoano ya kombe la mabingwa wa ulaya.
Timu ya Chelsea ya Uingereza imekumbana na kichapo kwenye uwanja wa San Siro jijini Milan kwenye mechi ya kwanza ya mtoano dhidi ya Inter Milan ya Italia ambayo hivi sasa inafundishwa na Jose Mourinho ambaye zamani aliwahi kuwa kocha wa Chelsea.

Inter walifanikiwa kuliona lango la Chelsea mapema kwenye dakika ya tatu ya mchezo kupitia kwa Diego Milito.

Chelsea walijipanga vyema baada ya bao hilo na kuanza kulisakama lango la Inter lakini juhudi zao zilizaa matunda kwenye kipindi cha pili pale Solomon Kalou alipoipatia Chelsea goli la kusawazisha.

Hata hivyo furaha za wapenzi wa Chelsea hazikudumu dakika nyingi kwani Esteban Cambiasso alifanikiwa kuipatia Inter goli la pili na la ushindi kwenye mechi hiyo.

Timu hizo zitarudiana tena kwenye uwanja wa Stamford Bridge jijini London baada ya wiki tatu.

source nifahamishe

No comments:

Post a Comment