Tuesday, February 16, 2010

Manchester Yaizamisha AC Milan 3-2, Real Madrid Hoi Ufaransa


Wayne Rooney ameendeleza wimbi lake la kuifungia mabao muhimu Manchester United kwa kuifungia Manchester United magoli mawili yaliyoisaidia kuibanjua AC Milan 3-2 kwenye uwanja wake wa San Siro. Real Madrid nayo imeshindwa kutamba na kupokea kichapo toka kwa Lyon ya UfaransaManchester United imejiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwa kujipatia ushindi mnono wa mabao 3-2 dhidi ya AC Milan kwenye uwanja wa San Siro.

Ronaldinho aliitanguliza AC MIlan mbele kwa goli safi kwenye dakika ya tatu tu ya mchezo huo lakini Paul Scholes aliisawazishia Manchester kwenye dakika ya 36.

Wayne Rooney alibadilisha upepo wa mechi kwenye kipindi cha pili kwa kuifungia Manchester magoli mawili na kuwafanya wenyeji AC Milan wawe nyuma kwa mbao 3-1.

Clarence Seedorf aliyeingia uwanjani kuchukua nafasi ya David Beckham aliipatia AC Milan goli la pili dakika tano kabla ya mechi kuisha.

Hadi kipyenga cha mwisho kinapulizwa, Manchester United iliondoka uwanjani ikiwa na ushindi wa mabao 3-2 na faida ya magoli ya ugenini ikiwasubiri AC Milan kwenye mechi ya marudiano kwenye uwanja wa Old Traford.

Katika mechi nyingine ya kombe la mabingwa wa ulaya, Real Madrid ya Hispania ikiingiza uwanjani kikosi chake cha wachezaji ghali duniani, ilishindwa kutamba nchini Ufaransa na kubugizwa 1-0 na timu ya Lyon.

Goli lililoizamisha Real Madrid lilifungwa na Jean Makoun kwenye dakika ya 47.

source nifahamishe

No comments:

Post a Comment