Wednesday, February 24, 2010

Ronaldo Kustaafu Soka Mwakani


Nyota wa Brazili, Ronaldo de Lima ametangaza mpango wake wa kustaafu kucheza soka na kutundika daluga zake mwakani.
Ronaldo ambaye kwa sasa anaichezea timu ya Corinthians ya jijini Sao Paulo nchini Brazili, ametangaza kustaafu kucheza soka la kulipwa ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao.

Ronaldo ambaye aliwahi kuchaguliwa mara tatu kuwa mchezaji bora wa dunia hivi sasa ana umri wa miaka 33.

Ronaldo alisema kuwa atastaafu kucheza soka lakini ataendelea kuiwakilisha Corinthians baada ya kustaafu kama balozi wake.

"Nimeongeza mkataba wangu kwa miaka miwili natarajia ndio miaka miwili ya mwisho katika soka", alisema Ronaldo.

Ronaldo ambaye aliibeba Brazili kutwaa kombe la dunia mwaka 1994 na 2002 hakuweza kuyaficha matumaini yake ya kuitwa kwenye kikosi cha Brazili kitakachoshiriki kombe la dunia baadae mwaka huu nchini Afrika Kusini.

"Tutaona itakavyokuwa, bado nina nifasi ya kuitwa timu ya taifa" alisema Ronaldo na kuongeza "Kwa kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazili itakuwa vigumu sana kwangu kushiriki kwani umri wangu utakuwa umesogea sana".

source nifahamishe

No comments:

Post a Comment